MWENGE WA UHURU WAWASILI JIJINI DAR ES SALAAM, MIRADI YENYE THAMANI YA SH. BILIONI 7 KUZINDULIWA
|
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam
Saidi Meck Sadik (kulia) akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa mmoja wa
wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bi. Tatu Saidi Mussa leo jijini Dar es
Salaam . Mwenge wa Uhuru umewasili jijini Dar es Salaam ukitokea Mkoa wa Kusini Pemba.
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO |
|
Mkuu wa wilaya ya
Temeke Bi. Sophia Mjema akiahidi mbele ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam
Saidi Meck Sadik kuupokea Mwenge wa Uhuru na kuukimbiza katika maeneo
mbalimbali ya wilaya hiyo ambapo miradi 11
itafunguliwa na kuwekewa mawe
ya msingi. |
|
Baadhi ya wafanyakazi
na wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam waliojitokeza kuupokea Mwenge wa
Uhuru katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo. |
|
Askari kutoka jeshi la Polisi wakiimarisha ulinzi wakati wa sherehe za mapokezi ya Mwenge wa Uhuru leo jijini Dar es Salaam. |
|
Wakimbiza Mwenge kitaifa wakiongozwa na kiongozi wa mbio za Mwenge Capt. Ernest Mwanossa (wa kwanza mbele) wakianza safari kuelekea maeneo mbalimbali ya wilaya ya Temeke leo jijini Dar es Salaam. |
|
Vijana wa halaiki kutoka wilaya ya Temeke wakiimba wimbo maalum wa Mwenge wakati wa mapokezi leo jijini Dar es Salaam. |
Posted by Editor
on 16:15.
Filed under
eastafricannews
.
You can follow any responses to this entry through the
RSS 2.0