Share this Post

dailyvideo

WANAFUNZI WATANO WAFARIKI NCHINI UGANDA BAADA YA MABWENI KUUNGUA MOTO.



Wanafunzi watano wameteketea kwa kuungua kwa moto nchini Uganda baada ya moto kuunguza mabweni mawili ya Leos Junior Academy katika manispaa ya Masaka.

Wanafunzi wote waliofariki ni wa elimu ya msingi ambao wameungua hadi kutotambulika, na miili yao imepelekwa katika hospitali ya rufaa ya Masaka.
Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Kusini Simon Peter Wafana amesema tayari polisi nchini humo imeanzisha uchunguzi wa chanzo cha moto huo.
Hii ni mara ya pili moto kuzuka katika shule hiyo katika kipindi cha miaka miwili.

Posted by Editor on 12:52. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for WANAFUNZI WATANO WAFARIKI NCHINI UGANDA BAADA YA MABWENI KUUNGUA MOTO.

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery