Share this Post

dailyvideo

YANGA YAICHAPA EXPRESS YA UGANDA 2-1


Kikosi cha Yanga
Wachezaji wa timu ya Yanga wakiingia uwanjani tayari kwa kumenyana na timu ya Express ya Uganda kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam
Mashabiki wa timu ya Yanga wakiwa wajaa uwanjani kushuhudia wachezaji wapya wa timu hiyo kwenye uwanja wa Taifa.
Mechi kati ya Yanga na Express ya Uganda,mpira umekwisha ambapo wenyeji Yanga wameshinda magoli 2-1, mabao yote yakitiwa kimiani na Jerry Tegete kipindi cha kwanza. Katika kipindi cha kwanza Yanga ilitawala mchezo kwa asilimia 60 dhidi ya Express hata hivyo katika kipindi cha pili mambo yamebadilika ambapo timu ya Express ya Uganda imefanikiwa kupata goli moja la kufutia machozi na kufanya matokeo kubaki hayohayo 2-1.
Kikosi kilichoanza Yanga, kutoka kulia waliosimama Ally Mustafa 'Barthez', Athumani Iddi 'Chuji', Said Bahanuzi, Oscar Joshua, Jerry Tegete na Nizar Khalfan. Walioinama kutoka kulia ni Kelvin Yondan, Nadir Cannavaro, Juma Abdul, Frank Damayo na Simon Msuva. 

Posted by Editor on 10:13. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for YANGA YAICHAPA EXPRESS YA UGANDA 2-1

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery