Share this Post

dailyvideo

Fid Q kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kula viazi vitamu

Fid Q enzi za utoto
Siku zote Fareed Kubanda aka Fid ni mtu anayependa kuwa unique katika mambo yake. Leo ikiwa ni siku yake ya kuzaliwa hapendi kusherehekea kama watu wengine walivyozoea kwa kuangusha party za gharama, kukata keki na kupop bottle kwa sana!
Kuonesha kwamba yeye ni ngoma halisi, Fid atasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kula viazi vitamu maarufu sana usukumani. Ukichanganya na maziwa ya mgando ama karanga zilizokaangwa, keki  haifui dafu! 
Fid ambaye siku yake ya kuzaliwa leo imemkuta kisiwani Ukerewe, ameiambia 255 ya XXL, Clouds FM kuwa amejisikia vibaya kukosa kituo cha yatima kujumuika na watoto katika siku yake hii muhimu.

Posted by Editor on 16:36. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Fid Q kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kula viazi vitamu

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery