Share this Post

dailyvideo

Hii ni Bab Kubwa: DJ Choka aamua kusheherekea birthday yake barabarani mitaa ya Morocco na watoto wa mitaani


Dj Choka

Dj wa wasanii na blogger maarufu hapa Tanzania Hugoline Martin anaefahamika zaidi kama Dj Choka leo Sept 19, 2012 ni siku anayokamilisha miaka 28 tangu ameanza kupumua.

Akiongea na Leotainment amesema anafuraha kubwa kuweza kuifikia siku ya leo na ameamua ku celebrate tofauti kwa kununua juice na keki kwa ajili ya kwendavyo  kusheherekea na watoto wa mtaani wanaopatikana maeneo ya Morocco Bagamoyo road.

Dj Choka alivyosheherekea birthday yake na watoto wa mitaani



Dj Choka amesema sababu ya kufanya hivyo ni kutokana na ndoto iliyomjia usiku wa leo ambapo aliota anakula na watoto yatima, so akajiuliza kwanini hii ndoto imekuja siku kama ya leo, na ndoto inamaana gani? Ndipo alipoamua kufanya kitu hicho. Choka amesema hana mpango wa kufanya party nyingine yoyote kwa leo kama ambavyo wengine hufanya kwa kualika friends na kula bata za kutosha.


Posted by Editor on 18:36. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Hii ni Bab Kubwa: DJ Choka aamua kusheherekea birthday yake barabarani mitaa ya Morocco na watoto wa mitaani

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery