Share this Post

dailyvideo

JUST IN: TFF YAMWENGUA MUHIDIN NDOLANGA

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) leo imetangaza kumwondoa 
Muhidin Ndolanga kwenye Kamati ya uchaguzi ya Chama cha Waamuzi nchini (FRAT) kwa 
kushindwa kuzingatia Katiba na taratibu za uchaguzi mkuu wa chama hicho ambao 
ulifanyika hivi karibuni mjini Dodoma.

Ndolanga ambaye mwaka jana alisimikwa kuwa mjumbe wa heshima wa TFF, ameenguliwa kuwa mwenyekiti wa Frat baada ya kukiuka Katiba ya FRAT ikiwa ni pamoja na maagizo ya Kamati ya Uchaguzi ya 
TFF chini ya Deo Lyato  iliyomtaka kusitisha uchaguzi huo kufatia baadhi ya taratibu 
kutokamilika jambo ambalo kiongozi huyo alilipuzia na kuendesha uchaguzi huo.

Kufuatia hali hiyo Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeamua kumchukulia hatua za kinidhamu 
kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi ibara ya 26 (8) kumwondoa kwenye kamati hiyo ikiwa 

ni pamoja na kumtaka Katibu mkuu wa TFF kumwasilisha kwenye Kamati ya Nidhamu  
ya Shirikisho hilo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaa, Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi wa TFF, Deo 
Lyato alisema kuwa uchaguzio huo uliofanyika hivi karibuni mjini Dodoma ni batili 

pamoja na viongozi wote waliochaguliwa ni batili na hawatumbuliki na TFF kwa kuwa 
haukuzingatia kanuni.
"Uchaguzi wa FRAT uliofanyika Novemba 17 Dodoma ni batili kwa kuwa haukuzingatia 
kanuni za uchaguzi za wanachama na maagizo ya TFF," alisema Lyato.

Alisema baadhi ya taratibu zilizokiukwa na Ndolanga ni kuwaruhusu wagombea ambao 

tayari walikuwa wameenguliwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF katika uchaguzi huo kwa 
kutokuwa na sifa.
Wagombea hao ni Omari Abdulkadir, Sudi Abdi pamoja na Ruvu Kiwanga ambao wawili 
kati yao walibuka na ushindi katika uchaguzi huo.
Hatahivyo Lyato alisema pia watu hao pia watafikishwa katika kamati ya Nidhamu ya TFF 
kwa mujibu wa ibara ya 26(8) ya kanuni za uchaguzi za wanachama wa shirikisho hilo 
kwa hatua za kinidhamu.

Posted by Editor on 17:40. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for JUST IN: TFF YAMWENGUA MUHIDIN NDOLANGA

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery