MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI, WASILIANA NAO SASA KWA NAMBA +255 757 361 266
Wanafunzi
wa mafunzo ya muziki wakiwa kwenye somo la matumizi ya viungo vya mwili katika kutengeneza midundo,
yaani “body percussion’ picha zote na AMTZ
****************************
****************************
ACTION MUSIC TANZANIA (AMTZ)
YAANZA KUTOA MAFUNZO YA UPIGAJI WA ALA ZA MUZIKI
‘MUSIC DECEMBER 2012’
Action Music Tanzania (AMTZ) ni asasi iliyosajiliwa na
BASATA na kupewa namba ya usajili BST/4733, imeanza kutoa mafunzo ya upigaji
ala za muziki kwa watu mbalimbali katika kipindi hiki cha likizo, yanayoitwa ‘Music
December 2012’
Mafunzo hayo ya upigaji wa ala za muziki ni kwa watu wote ambao
hawajaingia na wale waliokwishaingia katika tasnia ya muziki
lengo likiwa ni kuwafundisha na kuwajengea uwezo kimuziki
(muziki kama taaluma), ambapo mwanamuziki atajengewa uwezo wa kutunga,
kuandika, kusoma na kucheza ala kitaalam na jukwaani yaani ‘Live’
Mafunzo haya yanafanyika kuanzia mwezi disemba ili kutoa
fursa kwa wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi na sekondari kujiunga, pia
kuwapa nafasi watu walioko makazini kutumia fursa hii kujifunza muziki.
Mafunzo
ya upigaji ala za muziki kwa vitendo yatahusisha ala za muziki kama Kinanda
(piano,keyboard), Ngoma aina ya Konga, djembe na za mapipa, Tarumbeta ya Bb, Saxophone
ya Eb (alto sax), Gitaa la sauti ya juu (solo, rhythm) na chini (bass), Seti ya
Ngoma za Kimagharibi (drum set/kit) na Matumizi ya viungo vya mwili katika
kutengeneza midundo, yaani “body percussion’
Mafunzo
hayo yataambatana na nadharia ya Music ambapo mwanafunzi atajifunza namna ya
kuandika, kusoma na usikivu yaani ‘music writing, sight reading and ear
training’
Mafunzo
yanafanyika katika ofisi za Action Music Tanzania Mwenge, maeneo ya ITV, karibu
na Maryland bar – Shule ya Msingi Mwenge na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za
Maonyesho (FPA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mafunzo
yanatolewa na walimu wa muziki kutoka katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo
Kikuu cha Dodoma na kutoka kwenye bendi na taaisis nyingine za muziki hapa
nchini.
Fomu
za usajili zinapatikana ofisi ya AMTZ karibu na Shule ya msingi Mwenge kwa
shilingi za kitanzania 2,000/= tu. Njoo ujifunze kupiga ala za muziki kwa muda
mfupi na kwa bei nafuu.
Imetolewa
na
Mandolin
Kahindi
Katibu
Mtendaji-AMTZ
Tell:
+255 757 361 266




