Share this Post

dailyvideo

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 11, 2012
UCHAGUZI TWFA KUFANYIKA MOROGORO DESEMBA 19
Uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu kwa Wanawake Tanzania (TWFA) unatarajia kufanyika Desemba 19 mwaka huu mjini Morogoro.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, uchaguzi huo utatanguliwa na Mkutano Mkuu wa TWFA. Wajumbe wapiga kura wote wa mikoa iliyofanya uchaguzi wake na kutoa taarifa za uchaguzi wao ofisi za TWFA wanatakiwa kufika Morogoro siku moja kabla (Desemba 18 mwaka huu).
Wagombea waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ni kama ifuatavyo; wanaowania uenyekiti ni Isabela Kapera, Joan Minja na Lina Kessy. Rose Kissiwa ni mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti.
Wanaowania ukatibu mkuu ni Amina Karuma na Cecilia Mkafu. Nafasi ya mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inagombewa na Zena Chande pekee baada ya Furaha Francis kujitoa kutokana na sababu za kifamilia.
Sophia Charles na Triphonia Temba wanawania nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya chama hicho.
Wagombea Rahim Maguza, Macky Mhango na Rose Msamila wameondolewa kwa kushindwa kikidhi matakwa ya Katiba ya TWFA Ibara ya 28(2).
COASTAL YAANZA VIZURI MICHUANO YA KOMBE LA UHAI
Coastal Union ya Tanga imeanza vizuri michuano ya kuwania Kombe la Uhai inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Tanzania Prisons mabao 2-1.
Mechi hiyo ya kundi A imechezwa leo asubuhi (Desemba 11 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Coastal Union ilimaliza kipindi cha kwanza ikiwa tayari imepachika mabao hayo yaliyofungwa dakika ya 24 na 33 kupitia kwa Ramadhan Same na Yusuf Chuma.
Tanzania Prisons ambayo itacheza mechi yake pili kesho jioni (Desemba 12 mwaka huu) Uwanja wa Azam ulioko Chamazi dhidi ya JKT Ruvu ilipata bao lake dakika moja kabla ya filimbi ya mwisho.
Mechi nyingine za kesho ni Toto Africans dhidi ya Coastal Union itakayochezwa saa 2 asubuhi Uwanja wa Azam. Katika kundi B, Simba na African Lyon zitaoneshana kazi asubuhi Uwanja wa Karume wakati Azam na Polisi Morogoro zitacheza saa 10 jioni kwenye uwanja huo huo.
Kundi C kesho ni Kagera Sugar vs Oljoro JKT saa 2 asubuhi Uwanja wa Karume, na Yanga na Ruvu Shooting zitaumana saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Azam.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Posted by Editor on 13:36. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery