Share this Post

dailyvideo

FBI inayo miili ya magaidi wa Westgate


Mmoja wa magaidi walioshambulia Westgate
Mkuu wa majeshi ya Kenya ameabia vyombo vya habari kuwa shirika la Ujasusi la Marekani FBI lilikabidhiwa miili ya magaidi walioshambulia jengo la Westgate nchini Kenya mwaka jana.
Karangi, ameyasema hayoalipokuwa akikitoa maelezo katika mkutano ulioandaliwa nchini Kenya na baraza la vyombo vya habari kuhusu ambavyo shambulizi hilo lilishughulikiwa.
Magaidi hao walifyatua risasi kiholela na kuwaua takriban watu 67 huku mamia ya wengine wakijeruhiwa.
Bwana Karangi aliongeza kwamba baada ya shambulizi kuanza Jumamosi magaidi waliuawa siku iliyofuata.
''Miili ya magaidi hao ilikabidhiwa majasusi wa FBI,'' alisema Karangi ingawa hakutoa maelezo zaidi.
Washambuliaji wote wanne walikuwa wenye asili ya kisomali ingawa mmoja kati yao alikuwa ameishi zaidi nchini Norway
Maafisa wa usalama wakati huo wakipambana na magaidi hao walikuwa wametoa taarifa kuwa Westgate ilivamiwa na ilivamiwa na magaidi 12 ingawa idadi yao baadaye ilisemekana kuwa magaidi wanne pekee
Wanamgambo wa Somalia Al- Shabaab walidai kutekeleza mashambulizi hayo wakisema kuwa ilikuwa onyo kwa serikali ya Kenya kukoma kujihusisha na vita nchini Somalia ambako wanasadia majeshi ya Muungano wa Afrika kupambana dhidi ya Al Shabaab.
BBC SWAHILI

Posted by Editor on 09:20. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for FBI inayo miili ya magaidi wa Westgate

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery