MAMLAKA YA MAJI SAFI NA TAKA (DAWASCO) JE HIVI NDIVYO MLIVYO WAFUNDISHA WAFANYAKAZI WENU?
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Tukio hili limetokea jana ambapo Dada mmoja pamoja na vijana wa nne walifika katika nyumba moja maeneo ya Mwenge na Kukata Maji, cha ajabu baada ya kufika watu hao ambao walijitambulisha kuwa ni wafanyakazi wa DAWASCO na kuandika majina yao kuwa ni Augustino, Salim,Daston, Chambe, na Binti mmoja walikata maji na baada ya hapo walitoa risiti moja iliyotambulika kama (FOMU YA KUKATIWA MAJI)
Cha kusikitisha aliyekuwa anajaza fomu hiyo haijulikani kama ni kweli alikuwa ni Mfanyakazi kweli kutokana na alicho kiandika
Je swali linakuja kwa hawa Mamlaka ya maji safi na taka(DAWASCO), Hivi ndivyo walivyo wafundisha wafanyakazi wao kuandika pindi mteja anapo katiwa maji?
Soma mwenyewe hapa kilicho andikwa !