MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA KIWANDA CHA KUKAMUA MAFUTA YA UFUTA CHA TAKEMOTO, NAGOYA JAPAN NA BAADAE AHUTUBIA WASOMI JAPAN UMUHIMU WA VITEGA UCHUMI KWA MAENDELEO YA AFRIKA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa wa Kiwanda cha Mafuta ya Ufuta cha
Takemoto, Akira Ogawa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka kwa Ofisa wa Kiwanda cha kukamua mafuta ya Ufuta cha
Takemoto, Akira Ogawa, jinsi mbegu za ufuta zinavyoanza kuandaliwa
kuelekea katika mashine za kukamua mafuta. Hapa ni hatua ya kwanza
zinaposhushwa mbegu hizo na kuingia moja kwa moja kwenye mitambo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa wa Kiwanda cha Mafuta ya Ufuta cha Takemoto,
Akira Ogawa, jinsi mbegu za ufuta zinavyosafiri hadi kufika katika Kinu
cha kuzisaga hadi kupatikana mafuta hayo, wakati alipotembelelea
kiwanda hicho kilichopo Nagoya nje kidogo ya Jiji la Tokyo nchini Japan,
jana
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
na mkewe Mama Asha Bilal, wakionyeshwa mafuta ya ufuta na Ofisa wa
Kiwanda cha kukamua mafuta ya hayo cha Takemoto, Akira Ogawa, wakati
alipotembelelea kiwanda hicho kilichopo Nagoya nje kidogo ya Jiji la
Tokyo nchini Japan, jana
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
na mkewe Mama Asha Bilal, wakionyeshwa mbegu za ufuta na Ofisa wa
Kiwanda cha kukamua mafuta ya Ufuta cha Takemoto, Akira Ogawa, wakati
alipotembelelea kiwanda hicho kilichopo Nagoya nje kidogo ya Jiji la
Tokyo nchini Japan
Wakiendelea kutembelea kiwanda hicho.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu kiwanda hicho kinavyofanya kazi hadi
kupatikana mafuta ya Ufuta, wakati walipofika kiwandani hapo kujionea
kutembelea na kujionea shughuli za uzalishaji, jana Mei 22, 2014.
akiendelea kupata maelezo....
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal, mkewe Mama Asha Bilal, Balozi wa Tanzania nchini Japan, Salome Sijaona (wa pili kushoto) na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaki Okada, wakiongozana wakati
walipokuwa wakielekea kutembelea kiwanda cha kukamua mafuta ya Ufuta
cha Takemoto kilichopo Nagoya nje kidogo ya Jiji la Tokyo Japan, jana
Mei 22, 2014, akiwa katika ziara yake ya kikazi nchini Japan.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiagana na baadhi ya wanachuo Watanzania, wanaosoma katika Chuo hicho
baada ya kumalizika kwa Muahadhara huo jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akitoa muhadhara katika Chuo Kikuu cha Taaluma ya Sera 'GRIPS' wakati
alipoalikwa kwenye muhadhara huo uliofanyika chuoni hapo Jijini Tokyo
Japan, jana Mei 23, 2014.
Baadhi
ya wanachuo kutoka mataifa mbalimbali wa Chuo hicho waliohudhuria
Muhadhara huo, wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati alipokuwa
akitoa muhadhara.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiagana na baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini Japan,
waliohudhuria Muhadhara huo baada ya kumalizika kwa muhadhara huo katika
Chuo Kikuu cha Taaluma ya Sera 'GRIPS' Jijini Tokyo Japan, jana.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachuo Watanzania wanaosoma
katika Chuo hicho cha Taaluma ya Sera 'GRIPS' Jijini Tokyo Japan, jana
Mei 23, 2014, baada ya kumalizika kwa muhadhara huo. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
---
Na Mwandishi Maalum, Tokyo
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
amesema nchi zinazoendelea hususan za Kiafrika bado zinahitaji uwekezaji
zaidi vitega uchumi kutoka nje (FDIs) ili kupata maendeleo ya haraka
na kuondokana na umaskini.
Dkt.
Bilal ameyasema hayo leo (Mei 23, 2014) wakati akitoa muhadhara kuhusu
Mtazamo wa Nchi Zinazoendelea na Changamoto za Uwekezaji Vitega Uchumi
vya Nje na Hatma yake katika Kuondoa Umasikini kwa kutumia mfano wa
Tanzania ulioandaliwa na Taasisi ya Uchanganuzi wa Sera (GRIPS) mjini
Tokyo.
Alisema
Afrika inahitaji misaada zaidi itakayosadia kukuza teknolojia
itakayowawezesha Waafrika kuvuna maliasili ambazo hazijavunwa.
Aliongeza kuwa hii ndiyo njia pekee itakayoliwezesha Bara la Afrika
kuongeza mapato na kuchangia maendeleo ya haraka kwa wananchi wake.
Alisisitiza
kuwa uwekezaji unaohitajika zaidi ni katika sekta za za madini,
mafuta na gesi, kilimo na vyanzo vingine vya nishati kama vile nishati
ya jua na upepo. Alisema sekta hizo ndizo zinazohitaji teknolojia ya
kisasa kutoka mataifa yaliyoendelea ili kurahisisha uvunaji wake.
Wakichangia
hoja hiyo, wanafunzi wa chuo hicho walihoji namna Tanzania
inavyojiandaa kuhakikisha upatikanaji wa mafuta na gesi hauwezi kuathiri
amani na utulivu wa nchi yetu. Makamu wa Rais aliwaeleza kwamba
utafutaji, uchimbaji na usambaji unafanyika katika misingi ya uwazi ili
Serikali na kila mwananchi aelewe ni kwa namna gani atakavyonufaika na
rasimiali hiyo.