Share this Post

dailyvideo

Samsung kuwalipa fidia wafanyakazi wake


Wengi wa wagonjwa walipata Saratani ya damu au Leukemia
Kampuni kubwa duniani ya vifaa vye elektroniki, Samsung inasema kuwa itawalipa fidia wafanyakazi wake waliougua Saratani kutokana na kufanya kazi katika viwanda vyake.
Kampuni hiyo iliomba radhi kwa kesi ya muda mrefu kati yake na wafanyakazi hao waliokuwa wanadai fidia na badala yake kukubali kujiondoa katika kesi hiyo huku ikikubali kuwalipa fidia wagonjwa hao.
Hatua ya Samsung kukubali kuwalipa wafanyakazi hao inaleta matumaini katika kukamilika kwa mvutano huo ambao ulionekana kukwama kwa muda mrefu
Lakini afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo, Kwon Oh-hyun nusura kukiri kuwa kulikuwa sababu ya wafanyakazi hao kupatwa na Saratni ilichangiwa na wao kufanya kazi katika kiwanda cha Samsung. Wengi walipata Saratani ya damu au Leukaemia.
Baadhi ya bidhaa zinazotengezwa na Samsung Galaxy S5
Bwana Kwon alisema wafanyakazi kadhaa katika viwanda vyetu walipatwa na Saratani ya damu na kuugua magonjwa mengine yasiyokuwa na tiba ambayo yalisababisha baadhi yao kufariki.''
"tulipaswa kumaliza kesi hii kitambo sana na bila shaka tunahisi uchungu kwamba tulikosa kufanya hivyo, tunaomba radhi kwa hilo. ''
Akiongea na wandishi wa habari, Bwana Kwon alisema kuwa Samsung inatumai kuwa itaweza kumaliza kesi hii na kuweza pia kuwapa afueni wagonjwa na familia zao.''
Hata hivyo kampuni hiyo kubwa zaidi duniani ya simu za Smartphone haikusema idadi ya watu watakaolipwa fidia ingawa inaarifiwa ni watu 40 waliowasilisha malalamiko hayo huku kesi ikiendelea kwa zaidi ya miaka sita.

Posted by Editor on 19:52. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Samsung kuwalipa fidia wafanyakazi wake

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery