Share this Post

dailyvideo

Mazungumzo ya kutafuta amani nchini Kenya

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Kiasi ya watu ishirini waliuawa siku ya Jumapili katika eneo la Wajir kaskazini mashariki mwa Kenya kufuatia mapigano makali kati ya makabila hasimu katika eneo hilo linalopakana na Somalia.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
Kulingana na umoja wa Mataifa, kiasi ya watu 75,000 wameyatoroka makaazi yao katika miji ya Wajir na Mandera huku wengine 60,000 wakiathirika na mapigano hayo ya kikabila. Hapo jana viongozi wa kutoka eneo hilo walikutana na rais Uhuru Kenyatta kuzungumzia hali hiyo. Caro Robi amezungumza na mmoja wa washiriki wa mazungumzo hayo ya kutafuta amani Ugas Sheikh na kwanza ametaka kujua iwapo hali ya utulivu imerejea katika eneo hilo. Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mhariri: Caro Robi
Mwandishi: Mohammed AbdulRahman

Sauti na Vidio Kuhusu Mada

Posted by Editor on 17:13. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Mazungumzo ya kutafuta amani nchini Kenya

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery