Qatar kwenda kortini kuhusu 2022.
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Maafisa wa Qatar wanaaminika
kupanga mikakati madhubuti ya kukabiliana na tishio la kupokonywa
uenyeji wa kombe la dunia la mwaka wa Qatar 2022 kufuatia tuhuma za
rushwa .
Kamati andalizi ya michezo hiyo sasa inaaminika
kupania kufanya kila iwezalo ikiwemo kufuata mkondo wa kisheria, ikiwa
kura ya kuchagua mwandalizi wa kombe la dunia 2022,itarudiwa.Hata hivyo hatma yake imo mikononi mwa mchunguzi wa FIFA,Michael Garcia.
Mwanasheria huyo kutoka Marekani anatarajiwa kukamilisha uchunguzi wake itimiapo Juni 9.
Msimamo wake uko sawa na ule wa makamu wa rais wa Fifa, Jim Boyce aliyesema kuwa hatakuwa na shida yoyote ikiwa ‘makubaliano yatakuwa ni kura ya marudio kufanywa.’
Maafisa wa Qatari wanadai kuwa mtaji wa takriban pauni bilioni 23, mahsusi kwa ajili ya kombe la dunia la 2022, itapotelea mbali iwapo Fifa italipokonya taifa hilo la ghuba haki ya kuandaa michezo hiyo.