Share this Post

dailyvideo

Rais Kikwete akutana na Wataalamu watatu wa utafiti wa chanjo ya Malaria kutoka Ifakara Health Institute mjini Malabo, Equatorial Guinea

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

d3

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Dr. Ally Olot, mtafiti wa chanjo ya malaria na kiongozi wa watafiti wa Ifakara Health Institute (IHI) Malabo, Equatorial Guinea) walipomtembelea kwenye makazi yake mjini Malabo ambako Rais alikuwa anahudhuria mkutano wa kawaida wa Umoja wa Afrika. Wengine ni Dr. Mwajuma Chemba ambaye ni Mtalaamu mratibu wa tafiti za chanjo ya malaria, na Elizabeth Nyakarungu, Mtaalamu wa maabara, utambuzi wadudu wa Malaria).
d4
d6
Rais Kikwete aliwapongeza sana watafiti hao pamoja na taasisi ya IHI kwa kuiletea sifa Tanzania katika fani ya utafiti nje ya nchi.
Watafiti hao wako Equatorial Guinea (EG) kwa mwaliko wa serikali ya nchi hiyo kwa ajili ya kutoa msaada wa kitaalamu katika utekelezaji wa mradi wa utafiti wa chanjo ya malaria iitwayo PfSPZ na kuwafunza wenzetu kuhusu maarifa ya fani hii ya utafiti wa chanjo ya malaria. IHI ni shirika la utafiti lenye kufanya tafiti za afya nchini Tanzania lenye uzoefu wa miaka zaidi ya miaka hamsini. Mfano mmoja wa mafanikio yake ni utafiti uliopelekea vyandarua vyenye dawa kutumika kama moja wapo ya njia za kujikinga na malaria nchini Tanzania.
Tunafanya kazi pamoja madaktari na wataalamu kutoka Wizara ya Afya ya EG, shirika lisilo la kiserikali la Marekani liitwalo MCDI (Medical Care Development International) na Sanaria ambao ndio watengenezaji wa chanjo hiyo ya malaria.
Mradi huu wa utafiti  unagharamiwa na serikali ya EG pamoja na sekta binafsi za mafuta. Mradi huu wa miaka mitano una lengo la kuchunguza kuhusu uwezo wa chanjo hiyo kukinga dhidi ya ugonjwa wa malaria. Ushirikano huu ni mmoja ya mfano wa mashirikano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili kutafuta njia bora za kukinga maradhi katika jamii. Vilevile ni moja ya kielelezo kizuri cha jinsi gani nchi za kusini zinaweza kushirikiana katika taaluma mbali mbali (south south corporation).
Tumepata fursa ya kukutana na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshima Jakaya Mrisho Kikwete Malabo na kumueleza kuhusu kazi tunayofanya na changamoto mbalimbali zinazotukuta pamoja na kutoa ombi kwa mheshimiwa Rais kusahilisha mashirikano kati ya nchi mbili za Tanzania na Equatorial Guinea kupitia Wizara za Afya na Tume za Sayansi na technologia za nchi hizi mbili. Hili litafanya utelekelezaji wa mashirikiano hayo kuwa bora zaidi kwa lengo la kunufaisha nchi zote mbili.
Mashirikiano haya ni fursa ya watanzania kuwafunza wenzao pamoja na wao kujifunza kutokana na mashirikiano hayo. Utafiti huo pia utasaidia juhudi za kutokomeza ugonjwa wa malaria kwa kufanya tafiti zenye lengo la kutafuta chanjo bora ya malaria pamoja na njia bora za kusambaza chanjo hiyo kwa nchi zote mbili kama itakuwa ni yenye mafanikio.

Posted by Editor on 13:24. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Rais Kikwete akutana na Wataalamu watatu wa utafiti wa chanjo ya Malaria kutoka Ifakara Health Institute mjini Malabo, Equatorial Guinea

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery