Taarifa: Instagram yafuta rasmi picha za Uchi.
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ameambia BBC kuwa sheria zake kuhusu picha za uchi hazimbagui mtu yeyote.
Kampuni hiyo imekosolewa vikali kwa kwa kuondoa picha za wanawake walio nusu uchi kwenye mtandao huo.
Lakini Afisaa mkuu mtendaji wa
mtandao huo wa kijamii, Kevin Systrom, amesema kuwa sheria hizo
zinalenga kuhakikisha kuwa vijana na watu wazima wanaotumia mtandao huo
wako salama.
Masharti ya matumizi ya mtandao wenyewe,
yanasema: 'Mtu haruhusiwi kuweka picha za watu walio nusu uchi na picha
zenye mada ya ngono. ''
Matamshi yake yanakuja baada ya mwanawe
muigizaji maarufu, Bruce Willis, Scout Willis kuweka picha yake kwenye
mtandao huo akiwa nusu uchi bila kitu kifuani.
Picha hiyo iliondolewa kwenye mtandao huo na wamiliki wa mtandao na hapo ndipo malalamiko yalianza kuibuka.
Muimbaji Rihanna, ambaye alikuwa na wafuasi milioni 1.3 aliunga mkono kampeini hiyo kabla ya kufunga akaunti yake.
Wamiliki wa mtandao huo wanasema sheria zinapaswa kufuatwa na kila mtu awe mtu mashuhuri au vinginevyo.
"lengo letu ni kuhakikisha kuwa Instagram, ni mahala salama kwa kila mtu , awe maarufu au la. ''
"tunapaswa kuwa na sheria na kuhakikisha kuwa
kila mtu anafuata sheria hizo. Bila shaka tunapata changamoto nyingi
lakini tutnaedneklea kusisitiza umuhimu wa sheria kufuatwa, '' alisema
Systrom
Huku umaarufu wa mtandao huo ukiendelea
kuimarika, mtandao huo umekosolewa kuhusiana na baadhi ya picha
zinazochapishwa humo . Pia mtandao wenye umebana baadhi ya maneno
yanayohusiana na madawa ya kulevya.
Instagram ilinunuliwa na Facebook mwaka 2012.
BBC swahili
Posted by Editor
on 12:36.
Filed under
technology
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0