TIBA YA KUPONYA MAGONJWA MBALIMBALI KWA KUTUMIA UNYWAJI WA MAJI TU, MFUMO MZIMA NDIYO HUU
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Zaidi ya 90% ya magonjwa mengi mwilini ni matokeo ya sisi kutokunywa maji ya kutosha.
Je ni kiasi gani cha maji tunapaswa kunywa kila siku ?.
Kanuni
ya kimakisio kwa mahitaji ya maji ni; kunywa nusu ya uzito wako katika
aunsi (ounces) ugawe mara mfululizo utakaoufuata kwa siku nzima. Kiasi
kidogo chini au juu ya hiki, kinakubalika. Aunsi 1 = miligramu 31.25.
Kanuni
ya kimakisio kwa mahitaji ya chumvi ni, Robo tatu gramu za chumvi kwa
kila nusu lita ya maji, nusu kijiko cha chakula kwa kila nusu galoni ya
maji au kijiko kimoja cha chakula kwa kila galoni moja la maji.
Pengine umeshageuza kichwa na kujisemea, “Wewe ni kichaa…..hicho ni kiasi kingi sana cha maji”.
Ukweli
ni kuwa, ni rahisi kunywa hivyo hasa tukitumia sentensi, glasi 8 za
maji zikigawanywa mara nane kwa siku (glasi 1 = ml 250 au robo lita).
Mfano, kwa mtu mwenye uzito wa kilogramu 75:
Badili kilogramu kwenda aunsi kwa kuzidisha mara 2.2. Hivyo, 75×2.2 = aunsi 165.
Tafuta nusu ya aunsi kwa kugawa aunsi na 2. Hivyo, aunsi 165/2 = aunsi 82.5.
Gawanya mara mfululizo utakaoamua kuufuata kwa siku nzima, mfano mara 8 kwa siku. Kwa hiyo aunsi 82.5/8 = aunsi 10.3.
Badili aunsi kuwa miligramu za maji. Aunsi 1 = miligramu 31.25. Kwa hiyo aunsi 10.3×31.25 = miligramu 322.
Kwa hiyo itampasa mtu huyo mwenye uzito kilo 75, kunywa ml 322 za maji mara nane kwa siku.
Namna anavyopaswa kufuata hiyo ratiba mara 8 kwa siku:
1) Akiamka tu (mfano saa 12 kamili asubuhi), cha kwanza atakunywa maji ml 322. ataendelea na shughuli zake za asubuhi
2)
Nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi (yaani saa 12:30 asubuhi),
atakunywa maji ml 322. atasubiri nusu saa ipite ndipo atapata chakula
chake cha asubuhi (itakuwa saa 1 kamili asubuhi).
3) Kisha kula chakula cha asubuhi, atahesabu masaa 2 na nusu ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 3 na nusu asubuhi).
4)
Atahesabu masaa 2 tena ndipo atakunywa tena ml 322 nusu saa kabla ya
chakula cha mchana (itakuwa saa 6 mchana) kwa hiyo nusu saa baadaye
atakula chakula cha mchana (yaani saa 6 na nusu mchana).
5) Atahesabu yapite masaa 2 na nusu baada ya chakula cha mchana ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 9 kamili alasiri).
6)
Atahesabu masaa 2 na nusu yapite ndipo atakunywa maji ml 322 nusu saa
kabla ya chakula cha jioni (itakuwa saa 11 na nusu jioni). Nusu saa
baadaye atakula chakula cha jioni (itakuwa saa 12 kamili jioni).
7) Kisha kula chakula cha jioni, atahesabu masaa 2 na nusu tena ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 2 na nusu usiku).
Muda wowote atakapokwenda kulala kuanzia saa 4 usiku atakunywa tena maji ml 322 kumalizia mara 8 zake kwa siku.
Huyo
alikuwa na kilo 75, sasa na wewe andika uzito wako na utumie fomula
hiyo hapo juu ujuwe ni kiasi gani cha maji unahitaji kwa siku na kisha
ufuate mara hizo 8 kama zilivyopendekezwa hapo juu. Kwa staili hii ndipo
maji huwa ni zaidi ya dawa.
Kila mmoja wetu sasa anaweza kutumia uzito wake kwa kutumia fomula hii na kujua ni kiasi gani cha maji anahitaji kwa siku.
Kumbuka,
Kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ni kiasi cha chini kabisa,
lakini mahala pazuri pa kuanzia, ikiwa ni mtu unayejishughurisha zaidi
na mazoezi au unaishi katika mazingira ya joto zaidi, utahitaji zaidi ya
hapo.
Sasa, hutakubali kuwa kunywa maji kwa protokolo hii ni kazi rahisi?.
Ikiwa
haunywi kiasi hiki cha maji kwa sasa, unapaswa kuanza kuongeza kiasi
cha ziada kwa taratibu sana. Hii itaupa nafasi mwili kujirekebisha
kuendana na kiasi ulichoanza kukiongeza, na ikiwa hautaupa mwili muda wa
kujirekebisha, basi maji yatakuwa kama dawa ya kukojosha (diuretic),
yakisukuma madini na vitamini za mhimu nje ya mwili, pengine na
kukusababishia madhara zaidi kuliko faida.
Watu wazee na watoto wadogo wanatakiwa kuanza kuongeza maji kufikia mahitaji yao kwa taratibu zaidi.
Kwa
kutumia mfano wa uzito hapo juu, itakupasa kuanza na glasi 3 siku ya
kwanza huku ukiongeza glasi moja zaidi kila siku inayofuata mpaka ufikie
glasi zote 8.
Kumbuka kuwa, kunywa maji nusu ya uzito wako
katika aunsi na kula chumvi robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji,
ni kanuni ya kimakisio tu. Baadhi ya wengine watahitaji maji zaidi
wakati wengine watahitaji chumvi zaidi. Baada ya muda, mahitaji ya mwili
kwa maji na chumvi yanaweza kuongezeka kidogo zaidi sababu ya mazingira
ya joto, mazingira ya baridi au mazoezi ya viungo.
Kila mmoja lazima apate kujua kiasi cha mahitaji ya mwili wake kwa maji kuanzia sasa.
Kamwe usinywe zaidi ya aunsi 33.8 (lita moja) za maji kwa wakati mmoja ukiwa umekaa au umesimama.
Watoto
wadogo kuanzia miaka 2 mpaka 12, hasa wale wepesi kujishughulisha na
mazoezi wanahitaji asilimia 75 mpaka 100 za aunsi za maji katika uzito
wao kwa sababu miili yao inakua muda wote na kila seli katika miili yao
inayokua inayahitaji maji haya ya ziada (mytosis).
Fomula hii ya kunywa maji haitumiki kwa watoto chini ya miaka 2.
Chumvi
ya kawaida ya mezani iliyoongezwa madini ya iodini, itakusaidia kidogo,
chumvi ya mawe ya baharini ambayo haijasafishwa (unrefined sea salt)
ndiyo nzuri zaidi sababu ya madini mengine mengi ya ziada zaidi ya 80
yaliyomo ndani yake. Chumvi ya baharini pia huwa na radha nzuri, nyeupe
na umajimaji kidogo.
Namna bora za kula chumvi:
Njia
ya kwanza ni kuiweka chumvi katika sehemu ya mbele ya ulimi, hakikisha
unaihisi radha yake, na kisha kunywa maji juu yake yakiisafisha kuelekea
chini.
Unaweza pia kuongeza chumvi ya ziada kwenye chakula
chako.Tatizo la njia hii ni kuwa, chakula kinahisika kuwa na chumvi
zaidi ya radha zingine.
Ukiona viwiko, vidole, miguu, mikono
au kope za macho zinavimba (kuvimba kusikotokana na ajali au jeraha), au
unaharisha zaidi, usitumie chumvi kwa siku 2 mpaka 3, kunywa maji
halisi pekee na kisha siku ya tatu, endelea kuchukuwa chumvi tena,
lakini ichukuliwe taratibu. Kamwe usitumie chumvi zaidi ya robo tatu
gramu kwa kila nusu lita ya maji.
Kumbuka chumvi ikizidi hupelekea kuharisha.
Dr.Batmanghelidj
anasema, kunywa maji matupu kunaweza pelekea mwili kupoteza baadhi ya
madini na vitamini zake mhimu nje ya mwili na hivyo kutozipa seli muda
wa kutosha kuyatumia maji. Inashauriwa kutumia vidonge vyenye vitamini
nyingi kwa pamoja (multivitamins) katika kila mlo wako ili kurudishia
kile kitakachokuwa kimepotea (hasa ikiwa haufanyi mazoezi na kula kiasi
kingi cha mboga za majani).
Uvimbe utakapokuwa umepotea au
umeacha kuharisha, unaweza kuendelea na mpango wako wa kunywa maji nusu
ya uzito wako katika aunsi ingawa mara hii utayachukua kwa kiasi kidogo.
Kwa
siku nzima, anza kuongeza kiasi cha unywaji wako wa maji mpaka ufikie
tena nusu ya uzito wako katika aunsi, anza pia kuchukua chumvi pamoja na
maji. Unatakiwa kuhakikisha kuwa unapata gramu 150 za madini ya iodine
kwenye “multivitamins” zako kila siku mpaka gramu 450 kwa siku.
Kisha
kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa 2 mpaka 2 na
nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.
Ikiwa
inakulazimu kukojoa (peeing) chini ya muda wa masaa 2 tangu unywe maji,
utalazimika kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi
(uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, ya limau au ya zabibu au juisi
nyingine yeyote isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao
hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa.
Wakati huo huo mhimu kukumbuka kuongeza robo tatu gramu za chumvi katika kila nusu lita ya juisi yako.
Ikiwa
kunywa juisi hakutasaidia kupunguza kwenda bafuni kila mara, jaribu
kunywa maji huku ukila mkate. Unaweza kuongeza krimu ya siagi au jamu
kwenye mkate wako (the magic bagel).
Kisha kutumia mkate siku
moja au mbili unaweza kupunguza sasa kiasi cha mkate mpaka nusu yake,
robo yake na mwisho juisi pekee pamoja na mlo wako.
Utapaswa
kurudi taratibu tena kutoka kunywa maji juisi mpaka kunywa maji matupu
tena, baada ya siku kadhaa itakupasa kujaribu aunsi 2 za maji matupu
nusu saa kabla ya chakula, kesho yake aunsi 4, siku inayofuata itakuwa
aunsi 6 kisha 8 na kuendelea mpaka ufikie kiasi chako unachotakiwa.
Ikiwa
kunywa maji pamoja na kula mkate au katika juisi hakukusaidii kupunguza
kwenda bafuni, Glasi ya maji (ml 250) matupu ikiongezwa na kijiko
(kijiko cha chakula) kimoja cha asali au sukari halisi au walau sukari
nyeupe kutakutatulia tatizo hili ukiongeza na chumvi 1/8 ya kijiko cha
chai , tikisa na kisha kunywa mchanganyiko huo.
Bilashaka
umewahi kusikia msemo, “Kwa sehemu kubwa tumetokana na maji”, hii ndiyo
sababu zaidi ya asilimia 94 ya damu yetu ni maji, zaidi ya asilimia 85
ya ubongo wetu ni maji, huku zaidi ya asilimia 75 ya sisi ni maji.
Muda gani unywe maji fomula ya jumla:
Kitu
cha kwanza kufanya mara uamkapo tu, ni kunywa glasi 2 za maji (ml 500)
kwakuwa umetumia glasi 2 za maji kwa kulala mpaka asubuhi.
Kunywa
glasi 1 robo saa au glasi 2 nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi,
mchana na jioni, kisha hesabu masaa 2 au 2 na nusu kila baada ya chakula
cha asubuhi, mchana na jioni bila kunywa wala kula chochote, ndipo
unywe glasi 1 ya maji.
Kunywa glasi 1 ya maji kila uendapo kulala.
Muda wowote uamkapo usiku kwenda bafuni, kunywa nusu glasi ya maji na kipande cha chumvi kisha rudi kulala.
Muda wowote unapopatwa na kiu kunywa maji.
Kwanini unywe maji robo lita, robo saa kabla ya kula, au nusu lita, nusu saa
Chanzo: Juma Mtanda Blog