Share this Post

dailyvideo

Obama:Tumekadiria vibaya nguvu ya IS

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399


Rais Barack Obama wa Marekani
Rais Obama amekiri katika televishen ya kitaifa kuwa Mashirika ya Marekani yalikosea katika kukadiria hatari ya wapiganaji wa dola ya kiislam, Islamic State nchini Iraq na Syria.
Amesema kuwa wapiganaji hao wenye uhusiano na Al Qaeda walitumia fursa ya kutokuwepo serikali thabiti nchini Syria na kuongezewa nguvu zaidi na vijana waliojiunga kupigania jihadi kutoka mataifa mengine.
Hata hivyo Obama amesema wapiganaji hao waliwahi kuvurumishwa huko Iraq na majeshi ya nchi yake yakishirikiana na kabila la Sunni.
Obama amekiri vyombo vya Ujasusi vya Marekani zilikadiria vibaya uwezo wa majeshi ya Iraq kupambana na wapiganaji wa kiislamu ambao wameteka maeneo mengi nchini humo.

BBC

Posted by Editor on 14:47. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Obama:Tumekadiria vibaya nguvu ya IS

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery