Share this Post

dailyvideo

MKEMIA: MKOJO WA MASOGANGE UMEBAINIKA KUWA NA HEROIN

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

 
Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima, ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa sampuli ya mkojo wa msanii Agnes Gerald maarufu kama Deal ama Masogange (28) umebainika kuwa na dawa ya kulevya aina ya heroin.
 
Akitoa ushahidi leo Jumatano mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, shahidi huyo wa kwanza wa upande wa mashtaka, akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, ameiambia mahakama kuwa mnamo February 15, 2017 askari wawili kutoka Jeshi la Polisi Tanzania, Koplo Sospeter na WP Judith, walimfikisha Masogange ofisini kwake kwa lengo la kumfanyia vipimo vya mjono wake.
 
Alisema baada ya kuwapokea, alimsajili Masogange na kumpa namba ya mahabara 446 /2017 na kisha kuwakabidhi kifaa maalum kwa ajili ya kuweka sampuli ya mkojo.
Alidai baada ya kupokea sampuli ya mkojo ya Masogange alifanyia uchunguzi kwa kutumia kemikali na kubaini kuwa mkojo wake una chembechembe za dawa za kulevya aina ya heroin ambazo kwa kitaalamu zinajulikana kama Diacety Imophine.
 
Aidha, alisema uchunguzi zaidi ulibaini chembechembe za dawa nyingine ya kulevya aina ya Oxazepam.
 
Shahidi huyo alidai baada ya kufanya uchunguzi huo, aliandaa taarifa ya uchunguzi kuhusiana na sampuli hiyo ya mkojo ambapo aliisaini yeye mwenyewe na kuthibitishwa na kaimu mkemia mkuu wa serikali.
 
Shahidi huyo alimtambua Masogange kwa ndiye aliyepelekwa kuchukuliwa sampuli hiyo ya mkojo ofisini kwake

Posted by Editor on 10:58. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for MKEMIA: MKOJO WA MASOGANGE UMEBAINIKA KUWA NA HEROIN

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery