EAST AFRICAN NEWS

RAIS DKT MAGUFULI NA RAIS MUSEVENI WA UGANDA WAWEKA JIWE LA MSINGI LA BOMBA LA MAFUTA GHAFI, WAFUNGUA KITUO CHA PAMOJA CHA HUDUMA ZA MPAKANI MJINI MUTUKULA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Y...

10 Nov 2017 | 0 comments | Read more

WATANZANIA WANG'ARA SHINDANO LA MWANDISHI BORA WA SAYANSI NA KILIMO AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona (kushoto), akimkabidhi cheti Mwand...

29 Sep 2017 | 0 comments | Read more
ENTERTAINMENT NEWS

WAZIRI MWAKYEMBE AUDHURIA TAMASHA LA JAMAFEST NCHINI UGANDA

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe akipokelewa na Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ugand...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI (TASUBA) PAMOJA NA SHORT STATURE OF KENYA ZIKIONYESHA MAIGIZO TAMASHA LA JAMAFEST

 Kikundi cha burudani ya Uchekeshaji kutoka nchini Kenya maarufu kama Short Stature Society of Kenya kikitoa igizo lake la ku...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

DKT.MWAKYEMBE AMEWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI TAMASHA LA JAMAFEST KAMPALA, UGANDA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliy...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

WORLD NEWS

TECHNOLOGY

CONGRESS TO SMART DEVICE MAKERS: YOUR SECURITY SUCKS

Four senators propose the "Internet of Things Cybersecurity Improvement Act,"...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

HUAWEI CAME REALLY CLOSE TO SELLING AS MANY PHONES AS APPLE

Apple sold 41 million iPhones in the second quarter, while Huawei's shipments were a...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

SECRET SERVICE WILL REPORTEDLY TEST DRONE FOR TRUMP SECURITY

The Secret Service is looking at whether unmanned aerial vehicles could be use...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

WHAT APPLE'S EARNINGS TELL US ABOUT THE IPHONE 8

The iPhone 7 and 7 Plus may see it's future sibling sooner than many expected.  S...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more
CELEBRITIES NEWS

JOCKTAN MAKEKE KUSHIRIKI MAONESHO YA UTAMADANI NCHINI NIGERIA

 Mkurugenzi wa bodi ya Utalii nchini, Tanzania Devotha Mdachi  akikabidhiwa bendera Msanii wa mitindo, Jocktan...

09 Sep 2017 | 0 comments| Read more

IMPRESSIVE! BEYONCE LOOKS SLENDER IN LOW-CUT DRESS ON SUSHI DATE IN LA WITH JAY Z

Crazy in love: Beyonce looked absolutely fabulous on a sushi date night with husband Jay Z on Wednesday ...

04 Aug 2017 | 0 comments| Read more

BLOODIED JESSICA BIEL SIZZLES IN STEAMY SEX SCENE WITH HER HUNKY ONSCREEN HUSBAND

Bloody: The gimmick of the show is figuring out why this mother and wife decided to stab a man to death in the first place ...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

Share this Post

SPORTS NEWS

JOSEPH KIMWAGA KUKAA NJE MIEZI MINNE BAADA YA UPASUAJI WA GOTI

WINGA wa Klabu ya Azam FC Joseph Kimwaga akiwa katika chumba cha matibabu katika Hospitali ya Vincent Palloti iliyopo jijini ...

06 Sep 2017 | Read more
HEALTH NEWS

PAMOJA NA UNENE LAKINI HAWEZI ACHA KULA

The Brazilian boy, known only as Misael, was born a healthy 6lb 6oz (2.9kg) But every month since, has gained 6lb (3kg), meaning he str...

29 Sep 2014 | Read more
TOP TEN

Top 10 ‘Breaking Bad’ Moments

Ursula Coyote / AMC 10. The ricin’s fate is revealed For all its discussion over the course of the series, ricin had never been ...

08 May 2014 | Read more
FACTS

WACHINA NOMA SANA

 Ukisikia Wachina balaa sasa hii ni moja wapo, Kiwanda Kimojawapo cha China kijulikanacho kwa jina la LandWind kimeibuka na Kutengene...

25 Nov 2014 | Read more
ENVIRONMENT NEWS

A CLIMATE CHANGE INSPIRED PROJECT LAUNCHES IN DAR ES SALAAM

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399 ...

04 Aug 2017 | Read more
FASHION

MH. CATHERINE MAGIGE AZINDUA RASMI DUKA LA ZURII HOUSE OF BEAUTY

. MBUNGE wa Viti Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Vijana , Mkoa wa Arusha Catherine Magige  leo amezindua rasmi  duka ...

12 Jan 2015 | Read more
HISTORY

MAKALA FUPI: Mwanamke aliyehukumiwa kifo Sudan ajifungua

Meriam Yehya Ibrahim Ishag aliadhibiwa kwa makosa mawili, zinaa na kuas...

28 May 2014 | Read more
TRAGEDY NEWS

JOCKTAN MAKEKE KUSHIRIKI MAONESHO YA UTAMADANI NCHINI NIGERIA

 Mkurugenzi wa bodi ya Utalii nchini, Tanzania Devotha Mdachi  akikabidhiwa bendera Msanii wa mitindo, Jocktan...

09 Sep 2017 | Read more

dailyvideo

DKT.MWAKYEMBE AMEWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI TAMASHA LA JAMAFEST KAMPALA, UGANDA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliyokuwa ikipigwa na Kikundi cha Sanaa na Utamaduni Tanzania (TaSUBA) katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza mjasiriamali wa Tanzania kuhusu baadhi ya bidhaa zilizopo katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea zawadi ya shati toka kwa mjasiriamali wa Tanzania mara alipotembelea banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye tai nyekundu) akiangalia moja ya ubunifu wa picha iliyochongwa na mjasiriamali wa Tanzania wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewapongeza Wajasiriamali wa Tanzania kwa ushiriki wao katika Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST.

Dkt. Mwakyembe ametoa pongezi hizo leo mjini Kampala nchini Uganda katika viwanja vya Mashujaa Kololo alipotembelea kujionea namna tamasha hilo lilivyopokelewa na wadau wake walioiwakilisha Tanzania wakiwemo wajasiriamali toka vikundi mbalimbali, vikundi vya ngoma, vikundi vya sanaa ya maigizo pamoja na baadhi ya wasanii.

Katika tamasha hilo, Dkt. Mwakyembe pia alipata fursa ya kutembelea baadhi ya mabanda ya wajasiriamali hao pamoja na kuongea nao huku akijionea bidhaa mbalimbali zinazouzwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jambo ambalo limemfurahisha sana hususani kwa upande wa watu kutoka Tanzania kwakuwa wamejaza mabanda yao kwa bidhaa kadha wa kadha.

“Tamasha hili linaonyesha utajiri mkubwa wa sanaa, utamaduni pamoja na bidhaa tulizonazo kama nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, na hapa tumekutana kwasababu tunabadilishana mawazo na kuonyeshana bidhaa mbalimbali za nchi zetu”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Aidha, katika ziara hiyo, Dkt. Mwakyembe amewatoa wasiwasi wajasiriamali hao kuhusu suala la upatikanaji wa masoko huku akiwaahidi kuwatafutia fursa ya kuwapeleka wajasiriamali hao pamoja na bidhaa zao Bungeni mjini Dodoma ili ziweze kupata soko kwa urahisi kupitia wabunge.

“Niwatoe wasiwasi wajasiriamali wote wa Tanzania mliohudhuria hapa, nitahakikisha kuwa pindi tunaporudi nyumbani nitatafuta wasaa wa kulishawishi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili nyie mpate nafasi ya kuleta bidhaa zenu katika viwanja vya Bunge ili basi Wabunge wapate kujua haswa vitu vizuri mlivyonavyo nah ii itawasaidia kuviuza kwa urahisi zaidi na kujipatia vipato vyenu”, aliongeza Dkt. Mwakyembe.

Sambamba na hilo, Dkt, Mwakyembe amewahakikishia wajasiriamali hao kuhusu suala la kujitangaza kupitia vyombo vya habari akisema kwamba, atajitahidi kutoa ushawishi kwa vyombo vya habari nchini ili viweze kuwapatia muda wa kuwatangaza wajasiriamali hao ili wapate kujulikana ikiwemo shughuli wazifanyazo.

“Nitahakikisha kuwa siku mnapopewa nafasi ya kuja viwanja vya Bunge basi mnapata muda wa kutosha katika vyombo vya habari ili mpate kujulikana, hivyo kila mmoja wenu naamini atapewa nafasi ya kufanya mahojiano kwa kujieleza shughuli azifanyazo na mahali anapopatikana na hii itawasaidia kupata masoko zaidi toka kwa watu mbalimbali”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Kwa upande wao wajasiriamali hao wameshukuru Waziri Mwakyembe kwa juhudi alizowafanyia hususani za kuhakikisha kwamba wanahudhuria kwa kiwango kikubwa katika tamasha hilo, lakini pia ahadi aliyowapa ya kuwapeleka Bungeni ili wakatangaze bidhaa zao na kuwatangaza katika vyombo vya habari nchini.

Tamasha la JAMAFEST lilianzishwa mwaka 2013 nchini Rwanda na baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kwa mwaka huu tamasha hilo linafanyika mjini Kampala nchini Uganda ambapo pia tamasha hili linatarajiwa kufanyika tena katika moja ya nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) mwaka 2019.

Posted by Editor on 12:12. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for DKT.MWAKYEMBE AMEWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI TAMASHA LA JAMAFEST KAMPALA, UGANDA

Post a Comment

Photo Gallery

Designed by Solaranlagen | with the help of Bed In A Bag and Lawyers