Share this Post

dailyvideo

Wastara Ashukuru Watanzania-"Baada ya Miezi Mitatu Sajuki Anaweza Kuanza Kuigiza"


Maombi ya watanzania pamoja na michango yao ya fedha vimesaidia kumfikisha mwigizaji Sajuki hapa alipo baada ya kupata nafuu kubwa toka apelekwe India kuitibiwa.

Wastara akizungumza exclusive na millardayo.com amesema Sajuki anaweza kuanza kuigiza hata sasa kwa sababu nguvu imesharudi, anaweza kutembea kwa muda mrefu na hata hali yake ya sasa imebadilika sana tofauti na mwanzo.

Amesema “baada ya miezi mitatu Sajuki anaweza kuanza kuigiza kama yeye mwenyewe atapenda na hata sasa hivi alipo pale unaweza kwenda nae location hana wasiwasi wowote ila kwa sababu ni mtu amefanyiwa upasuaji anahitaji kupumzika zaidi huwezi kutoka nae kwa sababu kuigiza inahitaji akili zaidi lakini baada ya miezi mitatu anaweza kuendelea na kazi”
kwenye sentensi nyingine Wastara amesema hawezi kuzuia Sajuki kupigwa picha za Tv na magazeti kwa sababu kupitia vyombo hivyo vya habari ndio walifahamu kwamba anaumwa na wakaamua kumchangia sasa ni lazima wajue pia anaendeleaje kupitia vyombo hivyo hivyo na sio kwamba anamdhalilisha
Source Bongo Flava Music Blog

Posted by Editor on 10:44. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Wastara Ashukuru Watanzania-"Baada ya Miezi Mitatu Sajuki Anaweza Kuanza Kuigiza"

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery