FBI inayo miili ya magaidi wa Westgate
Bwana Karangi aliongeza kwamba baada ya shambulizi kuanza Jumamosi magaidi waliuawa siku iliyofuata.
''Miili ya magaidi hao ilikabidhiwa majasusi wa FBI,'' alisema Karangi ingawa hakutoa maelezo zaidi.
Washambuliaji wote wanne walikuwa wenye asili ya kisomali ingawa mmoja kati yao alikuwa ameishi zaidi nchini Norway
Maafisa wa usalama wakati huo wakipambana na magaidi hao walikuwa wametoa taarifa kuwa Westgate ilivamiwa na ilivamiwa na magaidi 12 ingawa idadi yao baadaye ilisemekana kuwa magaidi wanne pekee
Wanamgambo wa Somalia Al- Shabaab walidai kutekeleza mashambulizi hayo wakisema kuwa ilikuwa onyo kwa serikali ya Kenya kukoma kujihusisha na vita nchini Somalia ambako wanasadia majeshi ya Muungano wa Afrika kupambana dhidi ya Al Shabaab.
BBC SWAHILI
