EAST AFRICAN NEWS

RAIS DKT MAGUFULI NA RAIS MUSEVENI WA UGANDA WAWEKA JIWE LA MSINGI LA BOMBA LA MAFUTA GHAFI, WAFUNGUA KITUO CHA PAMOJA CHA HUDUMA ZA MPAKANI MJINI MUTUKULA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Y...

10 Nov 2017 | 0 comments | Read more

WATANZANIA WANG'ARA SHINDANO LA MWANDISHI BORA WA SAYANSI NA KILIMO AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona (kushoto), akimkabidhi cheti Mwand...

29 Sep 2017 | 0 comments | Read more
ENTERTAINMENT NEWS

WAZIRI MWAKYEMBE AUDHURIA TAMASHA LA JAMAFEST NCHINI UGANDA

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe akipokelewa na Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ugand...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI (TASUBA) PAMOJA NA SHORT STATURE OF KENYA ZIKIONYESHA MAIGIZO TAMASHA LA JAMAFEST

 Kikundi cha burudani ya Uchekeshaji kutoka nchini Kenya maarufu kama Short Stature Society of Kenya kikitoa igizo lake la ku...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

DKT.MWAKYEMBE AMEWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI TAMASHA LA JAMAFEST KAMPALA, UGANDA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliy...

14 Sep 2017 | 0 comments| Read more

WORLD NEWS

TECHNOLOGY

CONGRESS TO SMART DEVICE MAKERS: YOUR SECURITY SUCKS

Four senators propose the "Internet of Things Cybersecurity Improvement Act,"...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

HUAWEI CAME REALLY CLOSE TO SELLING AS MANY PHONES AS APPLE

Apple sold 41 million iPhones in the second quarter, while Huawei's shipments were a...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

SECRET SERVICE WILL REPORTEDLY TEST DRONE FOR TRUMP SECURITY

The Secret Service is looking at whether unmanned aerial vehicles could be use...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

WHAT APPLE'S EARNINGS TELL US ABOUT THE IPHONE 8

The iPhone 7 and 7 Plus may see it's future sibling sooner than many expected.  S...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more
CELEBRITIES NEWS

JOCKTAN MAKEKE KUSHIRIKI MAONESHO YA UTAMADANI NCHINI NIGERIA

 Mkurugenzi wa bodi ya Utalii nchini, Tanzania Devotha Mdachi  akikabidhiwa bendera Msanii wa mitindo, Jocktan...

09 Sep 2017 | 0 comments| Read more

IMPRESSIVE! BEYONCE LOOKS SLENDER IN LOW-CUT DRESS ON SUSHI DATE IN LA WITH JAY Z

Crazy in love: Beyonce looked absolutely fabulous on a sushi date night with husband Jay Z on Wednesday ...

04 Aug 2017 | 0 comments| Read more

BLOODIED JESSICA BIEL SIZZLES IN STEAMY SEX SCENE WITH HER HUNKY ONSCREEN HUSBAND

Bloody: The gimmick of the show is figuring out why this mother and wife decided to stab a man to death in the first place ...

03 Aug 2017 | 0 comments| Read more

Share this Post

SPORTS NEWS

JOSEPH KIMWAGA KUKAA NJE MIEZI MINNE BAADA YA UPASUAJI WA GOTI

WINGA wa Klabu ya Azam FC Joseph Kimwaga akiwa katika chumba cha matibabu katika Hospitali ya Vincent Palloti iliyopo jijini ...

06 Sep 2017 | Read more
HEALTH NEWS

PAMOJA NA UNENE LAKINI HAWEZI ACHA KULA

The Brazilian boy, known only as Misael, was born a healthy 6lb 6oz (2.9kg) But every month since, has gained 6lb (3kg), meaning he str...

29 Sep 2014 | Read more
TOP TEN

Top 10 ‘Breaking Bad’ Moments

Ursula Coyote / AMC 10. The ricin’s fate is revealed For all its discussion over the course of the series, ricin had never been ...

08 May 2014 | Read more
FACTS

WACHINA NOMA SANA

 Ukisikia Wachina balaa sasa hii ni moja wapo, Kiwanda Kimojawapo cha China kijulikanacho kwa jina la LandWind kimeibuka na Kutengene...

25 Nov 2014 | Read more
ENVIRONMENT NEWS

A CLIMATE CHANGE INSPIRED PROJECT LAUNCHES IN DAR ES SALAAM

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399 ...

04 Aug 2017 | Read more
FASHION

MH. CATHERINE MAGIGE AZINDUA RASMI DUKA LA ZURII HOUSE OF BEAUTY

. MBUNGE wa Viti Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Vijana , Mkoa wa Arusha Catherine Magige  leo amezindua rasmi  duka ...

12 Jan 2015 | Read more
HISTORY

MAKALA FUPI: Mwanamke aliyehukumiwa kifo Sudan ajifungua

Meriam Yehya Ibrahim Ishag aliadhibiwa kwa makosa mawili, zinaa na kuas...

28 May 2014 | Read more
TRAGEDY NEWS

JOCKTAN MAKEKE KUSHIRIKI MAONESHO YA UTAMADANI NCHINI NIGERIA

 Mkurugenzi wa bodi ya Utalii nchini, Tanzania Devotha Mdachi  akikabidhiwa bendera Msanii wa mitindo, Jocktan...

09 Sep 2017 | Read more

dailyvideo

Mchakato waanza kutafuta kiongozi wa mpito Burkina Faso

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

CHANZO DW SWAHILI

Wanadiplomasia wanaowawekea shinikizo viongozi wa jeshi la Burkina Faso kukabidhi madaraka kwa raia, wameanza mchakato wa kumtafuta mtu atakayeongoza serikali ya mpito hadi uchaguzi utakapofanyika.
Mkutano wa wadau katika mchakato wa kutafuta serikali ya mpito ya Burkina Faso
Mkutano wa wadau katika mchakato wa kutafuta serikali ya mpito ya Burkina Faso
Mazungumzo hayo ya jana yalisimamiwa na Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria, John Dramani Mahama wa Ghana na Macky Sall wa Senegal, yakiwashirikisha maafisa wa jeshi, viongozi wa vyama vya kisiasa na wawakilishi wa asasi za kiraia.
Ingawa washiriki waliafikiana juu ya kuwepo kwa utawala wa mpito kwa kipindi cha mwaka mmoja, ambao utaongozwa na raia, hakukuwapo makubaliano juu ya kiongozi wa kipindi hicho. Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliwaachia jukumu hilo wahusika nchini Burkina Faso.
''Na mtaendelea hadi pale mtakapompata mtu kutoka nchi hii, mwenye haiba, heshima, uaminifu na uzalendo ambaye ataweza kuiongoza Burkina Faso hadi mwakani, kwenye uchaguzi huru, wa haki na wa kuaminika. Hilo ndilo jukumu tunalowaachia kutekeleza.'' Alisema rais Mahama.
Rai ya kuepuka vikwazo
Rais wa Ghana John Dramani Mahama akitoa rai katika mkutano huo
Rais wa Ghana John Dramani Mahama akitoa rai katika mkutano huo
Rais Mahama alisema anaamini mchakato wa kumpata kiongozi huyo hautachukuwa wiki kadhaa, na kueleza matumaini yake kwamba haitakuwa lazima kwa jumuiya ya kimataifa kuiwekea vikwazo Burkina Faso. Umoja wa Afrika uliwapa wanajeshi wa Burkina Faso muda wa wiki mbili kukabidhi madaraka kwa raia, la sivyo wakabiliwe na vikwazo vya kiuchumi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon aliunga mkono juhudi za marais hao kutafuta suluhisho la amani katika mzozo huo wa Burkina Faso. Msemaji wake Stephen Dujarric amesema Umoja wa Mataifa unashirikiana na Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, kutafuta suluhisho la kudumu linalowahusisha wadau wote nchini humo.
Hali kadhalika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema pia linaunga mkono mchakato huo, na kuwataka wanajeshi kukabidhi madaraka na kuheshimu katiba ya nchi bila kuchelewa.
Ishara ya mvutano
Luteni Kanali Isaac Zida anayeshinikizwa kukabidhi madaraka kwa viongozi wa kiraia
Luteni Kanali Isaac Zida anayeshinikizwa kukabidhi madaraka kwa viongozi wa kiraia
Hata hivyo katika kile kilichochukuliwa kama ishara ya kupanda kwa joto la mvutano katika mkutano huo, wanasiasa wa upinzani pamoja na wanaharakati walitoka nje baada ya maafisa wa chama kilichokuwa madarakani kuingia katika mkutano huo.
Kiongozi wa asasi za kiraia Mathias Tankoano alisema hawawezi kukaa chumba kimoja na watu wanaotuhumiwa kusababisha vifo vya watu ambao hata bado hawajazikwa, na kuongeza kuwa maafisa hao wanapaswa kuhukumiwa kwa vifo hivyo, na kwa hila zao dhidi ya katiba ya nchi ambazo zililipeleka taifa katika ghasia.
Taarifa zilizotolewa baadaye zilisema Assimi Kouanda, kiongozi wa chama cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore alikamatwa na polisi baada ya kutoa matamshi ambayo yanaweza kuvuruga utulivu wa umma.
Burkina Faso iliingia katika mzozo wiki iliyopita baada ya kuibuka kwa maandamano yenye ghasia, kufuatia hatua ya aliyekuwa rais wake Blaise Compaore kujaribu kubadilisha katiba ili aweze kugombea mhula mwingine, kuendeleza utawala wake wa miaka 27. Baada ya kiongozi huyo kuikimbia nchi, aliyekuwa naibu kamanda wa kikosi cha kumlinda, Luteni Kanali Isaac Zida aliteuliwa na jeshi kuchukua madaraka ya kuiongoza nchi hiyo.
Mwandishi: Daniel Gakuba/APE/AFPE
Mhariri:Josephat Charo

Posted by Editor on 21:06. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Mchakato waanza kutafuta kiongozi wa mpito Burkina Faso

Post a Comment

Photo Gallery

Designed by Solaranlagen | with the help of Bed In A Bag and Lawyers