Profesa maji marefu achafua hali ya hewa Bungeni Dodoma Jana
Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani maarufu kwa jina la Profesa Maji Marefu (pichani), leo amesema bungeni kuwa kipigo alichopata Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, kinastahili ili naye apate machungu wanayopata wagonjwa wengine mahospitalini.
Profesa Maji Marefu aliitoa kauli hiyo wakati akichangia hoja katika bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bungeni Dodoma.
Kauli hiyo ilisababisha tafrani kidogo bungeni, ambapo Spika wa Bunge, Mhe. Anne Makinda alilazimika kuingilia kati kumzuia Profesa Maji Marefu asiendelee kutoa kauli hiyo kwani jambo la madaktari bado liko mahakamani.
Habari kwa Hisani ya Michuzi Blog
Habari kwa Hisani ya Michuzi Blog
Posted by Editor
on 11:51.
Filed under
eastafricannews,
feature
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0