RWANDA YAISHUTUMU KONGO KWA KUSHAMBULIA HIMAYA YAKE.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Louise Mushikawabo.
Rwanda imevishutumu vikosi vya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo vinavyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa kwa kuishambulia himaya yake wakati wa mapambano na waasi karibu na eneo la mpakani.
Hata hivyo Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Louise Mushikawabo amekaririwa akisema kuwa nchi hiyo haina nia ya kulipiza kisasi kwa uchokozi unaofanywa na Kongo.
Aidha Mushikawabo amesema masuala ya Mashariki mwa Kongo ni muhimu mno na hayapaswi kugeuzwa kuwa mzaha.
Posted by Editor
on 11:52.
Filed under
eastafricannews
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0