MHE ZITTO KUZICHAPA NA RAY KATIKA MCHEZO WA NDONDI JULAY 7 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM.
MHE ZITTO KABWE KUONYESHANA UBABE NA RAY.
RAY KUZICHAPA NA MHE ZITTO KABWE.
|
Ray atakayezipiga na Mhe. Zitt
o Kabwe |
MHE IDDY AZAN KUZICHIPA NA JB.
JB ATAYEZICHAPA NA MHE IDDY AZAN.MHE HALIMA MDEE ATAONYESHANA KAZI NA WOLPER.
WOLPER ATAYEZICHAPA NA MHE HALIMA MDEE.
|
Mhe Esther Bulaya |
|
Aunty Ezekiel |
KATIKA kunogesha
Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7 kwenye uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano watapanda
ulingoni kuzichapa na wasanii wa Bongo Movie.
Kwa mujibu wa Rais wa Oganaizesheni ya
Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) Yasin Abdallah 'Ustaadh' siku hiyo
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe atapanda ulingoni ili
kuonyeshana kazi na Vincent Kigosi 'Ray' katika pambano la raundi nne.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan
yeye ataonyeshana kazi na Jacob Stephen 'JB'. wakati Mbunge wa Kawe,
Halima Mdee na Jacklyne Wolper wenyewe watapimana ubavu, kabla ya Ester
Bulaya kuchapana na Aunty Ezekiel michezo yote hiyo pia ikiwa ya raundi
nne.
Ustaadh, alisema katika kuhakikisha
mabondia hao hawaumizani ulingoni watavishwa vifaa maalum vya kukinga
vichwa vyao ili wasipate majeraha kichwani.
Rais huyo wa TPBO alisema mara baada ya
mapambano hayo ya utangulizi, itashuhudiwa michezo miwili ya kimataifa
kati ya mabondia Thomas Mashali na Francis Miyeyusho kuzichapa na
Wakenya Patrick Amote na Shadrack Machanje.
Pia maboindia Ramadhani Mkundi atapanda
ulingoni pia kupigana na Martin Richard, huku pia ikitarajiwa kuwepo kwa
burudani mbalimbali za muziki na mchezo wa soka kati ya wabunge
mashabiki wa Simba dhidi ya wale wenzao wa Yanga na Bongo Fleva kuumana
na Bongofleva.
Ustaadh alisema michedzo hiyo iliyoandaliwa
na Global Publishers ni maalum kwa ajili ya kuchanisha fedha za ujenzi
wa mabweni ya wanafunzi wa kike na kutoa wito wadhamini na watu
mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuchangia na pia kuhudhuria tamasha
hilo.
KWA HISANI YA JUMA MTANDA BLOG
Posted by Editor
on 09:18.
Filed under
sportnews
.
You can follow any responses to this entry through the
RSS 2.0
Hayo ni mapambano au ni show tu ,na maigizo ya wabunge wetu jemeni