Share this Post

dailyvideo

MHE ZITTO KUZICHAPA NA RAY KATIKA MCHEZO WA NDONDI JULAY 7 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM.

 
MHE ZITTO KABWE KUONYESHANA UBABE NA RAY.
RAY KUZICHAPA NA MHE ZITTO KABWE.
Ray atakayezipiga na Mhe. Zitt o Kabwe
MHE IDDY AZAN KUZICHIPA NA JB. 
JB ATAYEZICHAPA NA MHE IDDY AZAN.MHE HALIMA MDEE ATAONYESHANA KAZI NA WOLPER.
 
WOLPER ATAYEZICHAPA NA MHE HALIMA MDEE.




Mhe Esther Bulaya
Aunty Ezekiel



KATIKA kunogesha Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7 kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano watapanda ulingoni kuzichapa na wasanii wa Bongo Movie.
Kwa mujibu wa Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) Yasin Abdallah 'Ustaadh' siku hiyo Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe atapanda ulingoni ili kuonyeshana kazi na Vincent Kigosi 'Ray' katika pambano la raundi nne.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan yeye  ataonyeshana kazi na Jacob Stephen 'JB'. wakati Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Jacklyne Wolper wenyewe watapimana ubavu, kabla ya Ester Bulaya kuchapana na Aunty Ezekiel michezo yote hiyo pia ikiwa ya raundi nne.
Ustaadh, alisema katika kuhakikisha mabondia hao hawaumizani ulingoni watavishwa vifaa maalum vya kukinga vichwa vyao ili wasipate majeraha kichwani.
Rais huyo wa TPBO alisema mara baada ya mapambano hayo ya utangulizi, itashuhudiwa michezo miwili ya kimataifa kati ya mabondia Thomas Mashali na Francis Miyeyusho kuzichapa na Wakenya Patrick Amote na Shadrack Machanje.
Pia maboindia Ramadhani Mkundi atapanda ulingoni pia kupigana na Martin Richard, huku pia ikitarajiwa kuwepo kwa burudani mbalimbali za muziki na mchezo wa soka kati ya wabunge mashabiki wa Simba dhidi ya wale wenzao wa Yanga na Bongo Fleva kuumana na Bongofleva.
Ustaadh alisema michedzo hiyo iliyoandaliwa na Global Publishers ni maalum kwa ajili ya kuchanisha fedha za ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike na kutoa wito wadhamini na watu mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuchangia na pia kuhudhuria tamasha hilo.
KWA HISANI YA JUMA MTANDA BLOG

Posted by Editor on 09:18. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

1 comments for MHE ZITTO KUZICHAPA NA RAY KATIKA MCHEZO WA NDONDI JULAY 7 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM.

  1. Hayo ni mapambano au ni show tu ,na maigizo ya wabunge wetu jemeni

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery