Share this Post

dailyvideo

TAIFA STARS YAWASILI MARRAKECH KUKIPIGA NA MOROCCO JUMAMOSI SAA 5 USIKU KWA SAA ZA BONGO

Taifa Stars imewasili leo jijini Marrakech, Morocco tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa siku ya Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia katika hoteli ya Pullman, ambayo pia ilifikia timu ya Ivory Coast ilipotua nchini humo 

kucheza na Morocco. Stars imetua na kikosi cha wachezaji 21 wakati Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu watawasili leo- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana wakitokea Maputo, Msumbiji ambapo jana- Juzi 2 mwaka huu timu yao ya TP Mazembe ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho.
Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa ambapo Tanzania itakuwa saaa 5 usiku.

Sufiani Mafoto Blog

Posted by Editor on 16:21. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for TAIFA STARS YAWASILI MARRAKECH KUKIPIGA NA MOROCCO JUMAMOSI SAA 5 USIKU KWA SAA ZA BONGO

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery