NEWS ALERT: OKWI AJIANDAA KUJIUNGA NA KIKOSI CHA SIMBA .
Emmanuel
Okwi Jumamosi iliyopita alionekana uwanja wa Taifa akiwa na Baadhi ya
viongozi na Mashabiki wa timu ya Simba ambayo ilikuwa inacheza na Mbeya
City
Emmanuel Okwi akitoa alama ya dole gumba kwa mashabiki wakati wa mechi kati ya Simba na Mbeya city Fc
Emmanuel Okwi akiwa na mashabiki
Habari
zilizo chini ya kapeti kwa mashabiki wa soka nchini ni kuwa klabu ya
Simba inajiandaa kumrudisha kundini mshambuliaji wake wa zamani Emmanuel
Okwi alieuzwa kwa klabu ya Etoile du Sahel ya nchini Tunisia. Taarifa
zinasema kuwa Etoile haijatimiza makubaliano yake na Simba ambayo
ilikuwa ni kuilipa klabu hiyo dola 300,000 na hadi sasa malipo hayo
hayajafanyika. Emmanuel Okwi tayari ametua jijini Dar es Salaam.