Share this Post

dailyvideo

FAHAMU UNDANI WA MNYAMA NUNGUNUNGU.


Nungnungu ni wanyama wagugunaji wenye ngozi yenye miiba iliyochongoka wanayotumia kujilinda na maadui. Walienea katika ulimwengu wa sasa na ulimwengu wa zamani. Katika wanyama wagugunaji ni watatu kwa ukubwa, wakitanguliwa na capybara na buku. Nungu wana urefu kati ya sm 20 - 25. Uzito wao wakaribia kg 5.4 - 16. Wana umbo la duara, wakubwa na wataratibu kweli.



Nungunungu ni wanyama ambao huwa na rangi mbalimbali zikiwemo kijivu,nyeusi,kahawia ambayo imepauka kwa sababu ya rangi zake na kumfanya kuwa miongoni mwa vivutio vya utalii

Nungu wa dunia ya leo wanaumbo dogo (japokuwa nungunungu wa Amerika ya Kaskazini wanafikia kama sm 85 kwa maelfu na uzito wa kilogramu 18), 

Ni vigumu sana kuweza kuwaona kwa vile wanaishi kwa mashaka sana,maana mara tu wanapoonekana machoni pa watu hushambuliwa na kuwaua kwa sababu mbalimbali.Wengine huwaua kwa sababu ya kuwatuhumu kuwa wanakula mazao yao mashambani.Lakini wengine huwaua kwa sababu wanadai kuwa miiba yake ni dawa.

Nungunungu hupenda kuishi na kufurahia mazingira yenye mapori na misitu ili kujihadhali na ukatilii anaotendewa.Nivigumu sana kumpata mnyama kama Nungunungu katika sehemu zenye nyasi fupi fupi huwa huishi kwe sehemu zenye nyasi ndefu kwa ajili ya usalama wao.

ILI KUMFAHAMU ZAIDI BOFYA HAPA

Posted by Editor on 15:00. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for FAHAMU UNDANI WA MNYAMA NUNGUNUNGU.

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery