JE WAJUA? HUYU NDIYE KIRUKANJIA WA TANZANIA
Kirukanjia ni mnyama jamii ya wanyama wanaopatikana katika nchi za Djibout,Eritrea,Ethiopia,Kenya,Somalia,Sudan,Tanzania na Uganda.Kitaalamu Kirukanjia anajulikana kama Xerus rutilus.
Ni wanyama wanaopatikana katika maeneo ya kitropiki yenye vichaka vifupi vifupi, nyasi na katika maeneo ya miinuko yenye miamba.
Tanzania ni nchi mojawapo ambapo wanyama hawa wanapatikana.Chakula cha Kirukanjia ni mizizi,nafaka,matunda,wadudu,mayai ya ndege pamoja na wanyama wadogo sana.
Maadui wakubwa wa Kirukanjia ni binadamu kutokana na kuwindwa kwa ajili ya nyama kwa baadhi ya jamii lakini zaidi uharibifu wa makazi yao kutokana na uharibifu wa mazingira.
Uzazi wa Kirukanjia mara nyingi hauna muda maalumu.Hata hivyo,vichanga huonekana miezi ya Julai hadi Octoba katka mwaka.Mimba ya Kirukanjia huwa ni kwa siku 48 na vichanga hunyonyeshwa kwa siku 52.
KUMJUA ZAIDI KIRUKA NJIA HUYU .. BOFYA HAPA




