Share this Post

dailyvideo

JE WAJUA? HUYU NDIYE KIRUKANJIA WA TANZANIA


 Kirukanjia ni mnyama jamii ya wanyama wanaopatikana katika nchi za Djibout,Eritrea,Ethiopia,Kenya,Somalia,Sudan,Tanzania na Uganda.Kitaalamu Kirukanjia anajulikana kama Xerus rutilus.

Ni wanyama wanaopatikana katika maeneo ya kitropiki yenye vichaka vifupi vifupi, nyasi na katika maeneo ya miinuko yenye miamba.

Tanzania ni nchi mojawapo ambapo wanyama hawa wanapatikana.Chakula cha Kirukanjia ni mizizi,nafaka,matunda,wadudu,mayai ya ndege pamoja na wanyama wadogo sana.

Maadui wakubwa wa Kirukanjia ni binadamu kutokana na kuwindwa kwa ajili ya nyama kwa baadhi ya jamii lakini zaidi uharibifu wa makazi yao kutokana na uharibifu wa mazingira.

Uzazi wa Kirukanjia mara nyingi hauna muda maalumu.Hata hivyo,vichanga huonekana miezi ya Julai hadi Octoba katka mwaka.Mimba ya Kirukanjia huwa ni kwa siku 48 na vichanga hunyonyeshwa kwa siku 52.

KUMJUA ZAIDI KIRUKA NJIA HUYU .. BOFYA HAPA

Posted by Editor on 09:20. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for JE WAJUA? HUYU NDIYE KIRUKANJIA WA TANZANIA

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery