Share this Post

dailyvideo

JITAMBUE SASA: USIKUBALI KUACHIKA UKIWA KWENYE UCHUMBA


UJANA una mambo mengi lakini vijana wa zama hizi tumezidisha. Matukio ndani ya uhusiano ni mengi zaidi ya wakati uliopita. Kukutana na wanandoa wanaoachana baada ya miaka miwili tu ni jambo la kawaida siku hizi.

Si ajabu tena kusikia msichana amechumbiwa na amevalishwa pete kabisa lakini baada ya siku kadhaa anaachwa. Hii ni aibu! Utakuta msichana hadi anaingia kwenye ndoa, ameshavaa pete za uchumba kutoka kwa wanaume hata wanne tofauti!

Ni mabadiliko mabaya lakini yanayosababishwa na mfumo mpya wa maisha ya sasa. Ndugu zangu, lazima tujifunze mambo muhimu ya kufanya ili uhusiano uwe wenye maana.

Vilio vya wasichana wengi ni kuhusu kuvalishwa pete au kudumu kwenye uchumba kwa muda mrefu, lakini ghafla mwanaume anamuacha na kuanzisha uhusiano na mwingine.

Hebu tujiulize; ni tamaa za wanaume hao au tatizo lipo kwa wanawake wenyewe? Dada zangu, naomba mfahamu kuwa, wakati mwingine ninyi ndiyo husababisha matatizo na hatimaye kuachwa.
Je, nini cha kufanya? Hapa nitakupa mambo muhimu ya kukaa nayo mbali ili uweze kuingia kwenye hatua inayofuata – ndoa. Karibuni darasani.

PATA UHONDO ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Posted by Editor on 22:02. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for JITAMBUE SASA: USIKUBALI KUACHIKA UKIWA KWENYE UCHUMBA

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery