Machar kukutana na Rais Kiir wa Sudan Kusini
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar
wanakutana ana kwa ana kwa mara ya kwanza tokea kuzuka kwa mzozo nchini
mwao mwezi Disemba mwaka jana na kusababisha ukiukaji mkubwa haki za
binaadamu.
Kiongozi wa waasi Riek Machar akiwa mjini Addis Ababa,Ethiopia kwa mazungumzo na Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini. (09.05.2014)
Mazungumzo hayo yanafanyika Ijumaa (09.05.2014) katika makao makuu ya
Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia kufuatia juhudi za Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon na Waziri wa mambo ya nje wa
Marekani John Kerry ambap hivi karibuni walifanya ziara nchini Sudan
Kusini.
Machar kwanza alikutana na wanasiasa wanne waandamizi ambao serikali iliwatia mbaroni kwa madai ya kula njama ya kufanya mapinduzi kwa niaba yake na ambao wameachiliwa huru wiki mbili zilizopita.
Duru zilizo karibu na mazungumzo hayo zinasema Machar pia alikuwa na mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ambaye ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo na Ushirikiano baina ya serikali za Nchi za Mashariki mwa Afrika (IGAD) ambayo ilikuwa msuluhishi katika mazungumzo hayo ya amani.
Matumaini ya amani
Mmojawapo wa wanasiasa walioachiliwa huru Pagan Amum amesema ana matumaini thabiti ya kufikiwa kwa amani na umoja kwa nchi yao.Amum ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa chama tawala cha Sudan Kusini SPLM amesema wanasubiri kwa hamu kukutana na Rais Salva Kiir kumshawishi juu ya haja ya kukomesha vita hivyo.
Pande hizo mbili hivi karibuni zimekubaliana juu ya usitishaji wa mapigano wa mwezi mmoja ili kuwawezesha wakulima kupanda mazao yao, lakini hata hivyo mapigano yamekuwa yakiendelea.
Mashambulizi ya serikali yaendelea
Amesema "Rais Salva Kiir hayuko makini katika suala la kutafuta ufumbuzi wa kisiasa kwa mzozo huu.Anaamini katika kuwa na ufumbuzi wa kijeshi na ndio maana vikosi vyake vinafanya mashambulizi kila mahala."
Koang ameongeza kusema ili kuzungumzia amani kunahitajika kuwepo mazingira mazuri ya kufanya hivyo lakini serikali inaendeleza vita.
Mapambano ya kuwania madaraka kati ya Kiir na Machar yaligeuka kuwa umwagaji damu hapo kati kati ya mwezi wa Disemba wakati yalipozuka mapigano kati ya wanajeshi waliokuwemo kwenye makundi tafauti yanayowaunga mkono ya kabila Dinka na la Nuer. Maelfu ya watu wameuwawa katika mzozo huo na wengine zaidi ya milioni moja wamepotezewa makaazi.
Shirika la Kimataifa la Haki za Binaadamu la Amnesty International na Umoja wa Mataifa wiki hii wameyashutumu makundi hayo yanayohasimiana kwa kuchochea unyama unaofanyika kwa misingi ya kikabila ambapo baadhi ya vitendo hivyo vinaweza kuhusishwa na uhalifu dhidi ya ubinaadamu.
Mwandishi : Mohamed Dahman/ dpa/Reuters
Mhariri:Yusuf Saumu
DW SWAHILI
Machar kwanza alikutana na wanasiasa wanne waandamizi ambao serikali iliwatia mbaroni kwa madai ya kula njama ya kufanya mapinduzi kwa niaba yake na ambao wameachiliwa huru wiki mbili zilizopita.
Duru zilizo karibu na mazungumzo hayo zinasema Machar pia alikuwa na mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ambaye ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo na Ushirikiano baina ya serikali za Nchi za Mashariki mwa Afrika (IGAD) ambayo ilikuwa msuluhishi katika mazungumzo hayo ya amani.
Matumaini ya amani
Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry akiwa na Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini mjini Juba.(02.05.2014)
Wawakilishi wa Kir na Machar walikuwa wakikutana kwa miezi
kadhaa lakini viongozi hao wenyewe hawakuwahi kukutana ana kwa ana tokea
kuzuka kwa mzozo huo wa Sudan Kusini.Mmojawapo wa wanasiasa walioachiliwa huru Pagan Amum amesema ana matumaini thabiti ya kufikiwa kwa amani na umoja kwa nchi yao.Amum ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa chama tawala cha Sudan Kusini SPLM amesema wanasubiri kwa hamu kukutana na Rais Salva Kiir kumshawishi juu ya haja ya kukomesha vita hivyo.
Pande hizo mbili hivi karibuni zimekubaliana juu ya usitishaji wa mapigano wa mwezi mmoja ili kuwawezesha wakulima kupanda mazao yao, lakini hata hivyo mapigano yamekuwa yakiendelea.
Mashambulizi ya serikali yaendelea
Msemaji wa waasi Brigedia Generali Lul Ruai Koang (kushoto), na
Gatdet Dak(kulia) msemaji wa Machar wakizungumza na waandishi wa habari
Addis Ababa . (09.05.2014)
Brigedia Generali Lul Ruai Koang msemaji wa waasi amesema hata
kabla ya mkutano huo kuanza tayari wamekuwa wakipokea taarifa kwamba
vikosi vya serikali vinavishambulia vikosi vyao katika majimbo matatu.Amesema "Rais Salva Kiir hayuko makini katika suala la kutafuta ufumbuzi wa kisiasa kwa mzozo huu.Anaamini katika kuwa na ufumbuzi wa kijeshi na ndio maana vikosi vyake vinafanya mashambulizi kila mahala."
Koang ameongeza kusema ili kuzungumzia amani kunahitajika kuwepo mazingira mazuri ya kufanya hivyo lakini serikali inaendeleza vita.
Mapambano ya kuwania madaraka kati ya Kiir na Machar yaligeuka kuwa umwagaji damu hapo kati kati ya mwezi wa Disemba wakati yalipozuka mapigano kati ya wanajeshi waliokuwemo kwenye makundi tafauti yanayowaunga mkono ya kabila Dinka na la Nuer. Maelfu ya watu wameuwawa katika mzozo huo na wengine zaidi ya milioni moja wamepotezewa makaazi.
Shirika la Kimataifa la Haki za Binaadamu la Amnesty International na Umoja wa Mataifa wiki hii wameyashutumu makundi hayo yanayohasimiana kwa kuchochea unyama unaofanyika kwa misingi ya kikabila ambapo baadhi ya vitendo hivyo vinaweza kuhusishwa na uhalifu dhidi ya ubinaadamu.
Mwandishi : Mohamed Dahman/ dpa/Reuters
Mhariri:Yusuf Saumu
DW SWAHILI