Share this Post

dailyvideo

SUDANI: Makubaliano Ya Amani Yavunjwa Sudan Kusini


Vikosi vya serikali ya Sudan Kusini na waasi wanaendelea kupigana wakivunja makubaliano mepya ya amani na kufifiisha matumaini ya kumaliza miezi mitano ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Kiongozi wa waasi Riek Machar(kulia) na rais wa Sudan Kusini Salva Kiir(kushoto) wakipeana mikono kumuomba Mungu kabla ya kutia saini makubaliano ya amani mjini Addis Ababa May tisa iliyopita
Mapigano yamepamba moto katika jimbo tajiri kwa mafuta la Nile ya juu,kwa mujibu wa waziri wa ulinzi Kuol Mayang aliyesema vikosi vya serikali vimeamariwa" visende kupigana,lakini vijihami tu vikishambuliwa."
Tangu rais Silva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar walipotia saini makubaliano ya kuweka chini silaha ijumaa iliyopita,pande zote mbili zinaendelea kulaumiana kuanzisha upya mashambulio .
"Riek Machar havidhibiti vikosi vyake na wanamgambo wake wenye silaha nzito nzito wanaojulikana kama "Jeshi jeupe" wanaojipakaa jivu kama alama ya vita na wakati huo huo kuepusha wasitafunwe na mbu" wamewashambulia wanajeshi wa serikali,waziri wa ulinzi Manyang ameendelea kusema.
"Hivi si vikosi vya kawaida,jeshi jeupe limeundwa na raia na hawajaarifiwa chochote kuhusu makubaliano yaliyofikiwa ili kusitisha uhasama-waziri huyo wa ulinzi wa serikali ya mjini Juba amesema na kuongeza waasi ndio waliokuwa wa kwanza kushambulia.
Rais Silva Kiir anasema anataka amani
Wanajeshi wa Sudan Kusini waakishangiriwa na wananchi huko Malakal
Nae msemaji wa jeshi Philip Aguer amesema wasimamizi kutoka jumuia ya IGAD wanapelekwa Bentiu,mji mkuu wa jimbo tajiri kwa mafuta Unity .
Rais Salva Kiir amesisitiza alipokuwa akiuhutubia umati wa watu huko Juba kwamba anataka amani."Tumewaamuru wanajeshi wetu wasibanduke mahala walipo kuwashambulia waasi."Amesema.
Pande hizi mbili ziliwahi kukubaliana kuweka chini silaha mwezi january uliopita,lakini makubaliano hayo hayakukawia kuvunjika na wimbi jipya la mapigano kuripuka.
Wachunguzi wa mambo wanasema pande zote mbili zinakabiliwa na changamoto ya jinsi ya kutekeleza makubaliano ya amani huku muungano wa makundi ya wanamgambo yakiwaleta pamoja wanajeshi walioasi na makundi yanayohasimiana ya kikabila.
Pande zote mbili zinalaumiana kuwatumia mamluki na waasi kutoka nchi jirani ya Sudan huku upande wa serikali ukiungwa mkono na wanajeshi wa Uganda-Muundo wa Uongozi wa Kiir unatajikana pia kuwa dhaifu.
Uhalifu wa Vita na uhalifu dhidi ya ubinaadam
Kambi za wakimbizi huko Tomping-Juba
Vita katika nchi hii changa kabisa ulimwenguni vimeangamiza maisha ya maelefu ya watu-huku watu milioni moja na laki mbili wakilazimika kuyahama maskani yao.
Umoja wa Mataifa na mashirika yasiyomilikiwa na serikali yanalaani uhalifu wa vita na uhalifu dhidi ya ubinaadam uliofanywa na pande zote hizo mbili:mauwaji chini ya misingi ya kikabila,kulazimishwa watoto elfu tisa watumikie vitani,mashambulio dhidi ya shule na vituo vya huduma za afya,utekaji nyara wanawake na wasichana pamoja na ubakaji....
Mwandishi:Hamidou Oummilkheir/AFP
Mhariri: Mohammed Abdul-rahman

DW SWAHILI

Posted by Editor on 17:28. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for SUDANI: Makubaliano Ya Amani Yavunjwa Sudan Kusini

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery