Share this Post

dailyvideo

UKICHEPUKA MARA MOJA, INAWEZA KUYAGHARIMU MAISHA YAKO YOTE

Tukiendelea na mada yetu kutoka pale tulipoishia wiki iliyopita, suala la kuchepuka ni la kupiga vita. Anayekuja kwako na vishawishi vya hapa na pale ndiye adui yako pale mambo yanapogeuka. Ukichepuka utamuumiza sana mwenzio, kisha nawe utaumia.

Hii ni kwa sababu mateso ya mwenzi wako hayawezi kukupa ahueni. Kwa walio kwenye mapenzi ya dhati ni kwamba mwenzi wako anapoteseka, na wewe pia unakuwa kwenye mateso makali. Maana furaha yake ni yako, maumivu yake yanakugusa pia. Vivyo hivyo kilichopo kwako naye kinamhusu kwa tafsiri pana.

Juu ya hapo ni kuwa hisia za maumivu katika mapenzi zina kawaida ya kuhama kutoka upande mmoja kwenda mwingine. Unamtesa sana, siku akichukua uamuzi wa kusema “mwana kwenu kwa heri”, hapo ndipo unashtuka, eti huamini kinachotokea.

Maombi ya msamaha kutoka kwako kwenda kwake yanakuwa kwa unyenyekevu wa hali ya juu sana. Kwa nini mfike huko? Akili yako itumikishe kufanya uamuzi sahihi ambao ni kumtunza mwenzi wako ambaye anakutunza hivi sasa. Maudhi ya hapa na pale jiepushe nayo.

Mdharau mwiba guu huota tende! Usione anachokilalamikia mwenzi wako ni kidogo, mfanye afurahie uwepo wako kila siku. Usimruhusu akulilie, maana ipo siku utalia wewe. Hakikisha hatoi machozi ya maumivu, isipokuwa yawe ya furaha. Kinyume chake kuna siku yatakugeuka.

ASIMULIAYE MVUA IMEMNYESHEA
Maryam Zambi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 46. Ni mama wa watoto wanne, yupo kwenye ndoa kwa mwaka wa 19 sasa. Aliolewa na Raphael Zambi, 51, mwaka 1995. Akiwa na watoto wawili, aligundulika kuwa na uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa.


KUPATA UHONDO ZAIDI INGIA HAPA>>> 

GPL

Posted by Editor on 15:34. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for UKICHEPUKA MARA MOJA, INAWEZA KUYAGHARIMU MAISHA YAKO YOTE

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery