KUMBE SOMETIMES UONGO UNAHITAJIKA KWENYE MAPENZI!
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Somo la leo linashangaza kidogo lakini ni vizuri kama tukijifunza. Tumezoea kusikia kuwa uongo ni kitu kibaya katika maisha ya mwanadamu – ni kweli. Uongo si mzuri lakini katika uhusiano na mapenzi, wakati mwingine unanafasi na unaboresha sana uhusiano.
Kwa kawaida uongo unakatazwa kuanzia kwenye mafundisho ya dini na hata katika jamii. Mtu muongo si mwaminifu. Hakubaliki.
Hata mwanasiasa ambaye ni muongo, wapigakura wake hawamchagui tena atakaporudi mara ya pili; kwa nini? Kwa sababu aliwaongopea.
Hiyo ni kweli kabisa, lakini hapa katika Let’s Talk About Love nataka kukupa kitu kipya kabisa ambacho hujawahi kukipata mahali popote; uongo mtamu!
Ndiyo! Kuna uongo mzuri tena wenye faida na utakaokusaidia kukuza upendo wako kwa mwenzi wako. Ni suala la kukubali kujifunza tu. Karibu darasani tujifunze...
UDANGANYIFU
Rafiki zangu, sitaki kueleweka vibaya katika hili lakini kama nilivyosema mwanzo, uongo si kitu kizuri kwenye jamii. Mtu anayedanganya hakubaliki. Kwa tafsiri ya haraka, mwongo si mwaminifu.
Haaminiki kwa sababu ni rahisi kutunga mambo ambayo hayapo na akayatengenezea mazingira yakaonekana ni ya kweli. Huyu hafai hata kidogo. Lakini rafiki zangu, katika uhusiano upo uongo ambao unakubalika kama nilivyosema.
Nasema unakubalika maana una lengo la kutengeneza uhusiano, kuufanya uendelee kuwa na nguvu na si kuupoteza.
GPL
ENDELEA KUSOMA BOFYA HAPA>>>
Posted by Editor
on 10:21.
Filed under
loveandrelationships
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0