Share this Post

dailyvideo

Rais mpya wa Misri kuapishwa

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Raia wanaomuunga mkono Abdel Fatah al sisi
Usalama umeimarishwa katika mji mkuu wa Misri ,Cairo kabla ya kufanyika kwa sherehe ya kumuapisha rasmi rais mpya wa taifa hilo Abdel Fatah el Sisi.
Rais huyo mteule atakula kiapo chake cha kuchukua mamlaka katika mahakama kuu ya kikatiba mjini Cairo.
Alishinda uchaguzi wa urais wa mwezi uliopita kwa wingi wa kura ijapokuwa idadi ya waliojitokeza kushiriki katika shughuli hiyo ilikuwa chini ya asilimia 50.
Uchaguzi huo unajiri miezi michache tu baada ya kiongozi huyo kumpindua madarakani aliyekuwa rais wa taifa hilo Mohammed Morsi.
Mkuu huyo wa jeshi wa zamani ameanzisha msako dhidi ya wanaompinga mbali na kukipiga marufuku chama cha Morsi cha Muslim Brotherhood.
BBC

Posted by Editor on 12:44. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Rais mpya wa Misri kuapishwa

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery