Breaking news Hatari: Watu 30 wauawa katika shambulizi, Kenya
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Wizara ya maswala ya ndani nchini Kenya inasema kuwa takriban watu thelathini wameuawa katika mashambulizi mawili tofauti katika makaazi ya pwani ya kenya karibu na mpaka wa Somali.
Inadaiwa kuwa watu walikuwa wakitizama mechi za kombe la dunia wakati wa tukio hilo.
Shambulizi la pili lilitekelezwa karibu na eneo la Mpeketoni ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa katika shambulizi jengine mwezi uliopita.
Kundi la wapiganaji wa Al shabaab limekiri kutekeleza mashambulizi hayo.
BBC Swahili
Posted by Editor
on 11:09.
Filed under
eastafricannews,
feature
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0