Hatari zaidi Kenya: Mashambulizi mengine yatokea Lamu
Watu 300 waliokuwa wamejihami wamevamia kijiji cha Pandanguo katika Kaunti ya Lamu Pwani ya Kenya.
Chifu wa eneo hilo Karisa Charo Karisa, anasema
kuwa shule na nyumba nne ziliteketezwa katika mashambulizi hayo
yaliyofanywa usiku wa kuamkia leo ikiwemo shule moja ya msingi.Walivamia msikiti ambako polisi hao wa akiba walikuwa wanasali. Mmoja wa polisi hao aliyeponea kifo aliambia BBC kuwa waliambiwa wachague kati ya mauti na bunduki zao.
Hapo ndipo walilazimika kuwapa washambuliaji hao bunduki zao.
Kwa sasa hakuna taarifa zozote kuhusu majeruhi wa mashambulizi hayo.
Inaarifiwa kuwa wanajeshi wamepelekwa katika eneo hilo kudhibiti usalama.
Mnamo mwezi Juni watu watano waliuawa katika eneo hilo la Pandanguo ambalo liko umbali wa kilomita 30 kutoka Mpeketoni ambako mashambulizi mengine yaliwaacha watu zaidi ya sitini wakiwa wameuawa.
Waathiriwa wengi wa mauaji walipatwa wakiwa wamefungwa mikono nyuma ya migongo na koo zao zikiwa zimekatwa.
Eneo la Lamu ambalo liko Pwani ya Kenya limekuwa na mashambulizi ya mara kwa mara tangu mwezi Juni huku watu wakiuawa kwa misingi ambayo bado ni tata.
Mashambulizi ya Kwanza yaliyofanyika mjini Mpeketoni, yalisemekana kufanywa na kundi la wanamgambo la Al Shabaab ingawa serikali alilalaumu wanasiasa kuyachochea mashambulizi hayo.
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Posted by Editor
on 17:26.
Filed under
eastafricannews,
feature
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0