Share this Post

dailyvideo

AUNT EZEKIEL ASEMA: BIFU LANGU NA RAY, STEVE LIMEKWISHA

Na Shakoor Jongo
BIFU la muda mrefu lililokuwepo kati ya wasanii wa filamu, Aunt Ezekiel, Steven Mangere ‘Nyerere’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ limezimika baada ya mastaa hao kukaa na kuamua kumaliza tofauti zao.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni katika Pub yake iliyopo Mwananyamala jijini Dar, Aunt alisema bifu hilo lililowafanya kutoshirikiana katika mambo ya kimaendeleo kwa muda mrefu lilikuwa likiwaathiri sana hivyo wakaamua kukubali yaishe.
“Unajua kifo cha Kanumba ndicho kilichotufanya sisi waigizaji tuwe kitu kimoja na kumaliza tofauti zetu ndiyo maana unamuona Ray na Steve wako hapa kwenye Pub yangu kuonyesha ni jinsi gani tunaungana mkono katika masuala ya maendeleo na si kuwekeana chuki zisizo na maana,” alisema Aunt.
KWA HISANI YA GLOBAL PUBLISHERS 


Posted by Editor on 11:29. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for AUNT EZEKIEL ASEMA: BIFU LANGU NA RAY, STEVE LIMEKWISHA

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery