MWANAMKE MWENGINE MTANZANIA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA HUKO DUBAI
Mwanamke
mmoja ambaye ametambulika kuwa ni mtanzania amekamatwa kwenye airport
ya Dubai akiwa na dawa za kulevya aina ya Cocaine na alikuwa anatoka
Brazil kuja Tanzania ambapo baada ya kuhojiwa na Polisi wa Dubai, kasema
rafiki wa mme wake ndio alimuomba ampelekee mizigo yake nyumbani
Tanzania.
Huyu
mwanamke amesema alikuwa anatoka kwenye mapumziko ya miezi mitatu
ambayo aliandaliwa na mume wake huko Brazil lakini anavyorudi ndiyo
alipewa huo mzigo kuuleta Tanzania ambao ni dawa za kulevya aina ya
cocaine zenye thamani ya zaidi ya bilioni moja nukta tatu za
Tanzania(Dhs 3 million).
Alikamatwa wakati anajiandaa kubadilisha ndege ili kupanda inayokuja Tanzania.
Hakujatolewa taarifa nyingine zaidi ila millardayo.com inaendelea
kufatilia info zaidi kwa sababu bado Mtanzania huyu anashikiliwa na
polisi wa Dubai.
Hiyo picha imezibiwa hukohuko Dubai ilikopigwa.
Hili tukio limetokea siku kadhaa baada ya mabinti wa Kitanzania
kukamatwa wakiingiza dawa za kulevya kwenye nchi za Zimbabwe na Afrika
Kusini wakati pia kwenye Uwanja wa ndege Dar es salaam mwanaume
Mtanzania alikamatwa siku kadhaa zilizopita akiwa anasafirisha dawa za
kulevya.
CHANZO : VIJIMAMBO BLOG