Share this Post

dailyvideo

MUGABE ATIMIZA MIAKA 90


Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe leo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza umri wa miaka 90. Hata hivyo sherehe yake imegubikwa na wasiwasi juu ya afya yake.
Wakati ambapo wasaidizi wake wanasema afya yake iko vizuri, wiki hii alienda tena nchini Singapore kwaajili ya upasuaji wa macho na hivyo kuamsha tena wasiwasi. Bado yupo nchini humo na sherehe yake ya kuzaliwa itafanyika uwanjani siku ya Jumapili na inadaiwa kugharimu dola milioni 1.
Kiongozi huyo wa Zimbabwe tangu mwaka 1980, amekuwa akienda Singapore kutibiwa mara kadhaa.
Mugabe alizaliwa tarehe 21 February 1924. Sherehe yake itahudhuriwa na maelfu ya wananchi kwenye uwanja wa Marondera, mji uliopo kilomita 75 mashariki mwa mjini mkuu, Harare.
Kutakuwepo na muziki, michezo na chakula

Posted by Editor on 16:05. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for MUGABE ATIMIZA MIAKA 90

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery