HABARI MPASUKO: NDEGE YA MALAYSIA MH370 ILIANGUKA BAHARI YA HINDI NA KUSABABISHA VIFO VYA ABIRIA WOTE WALIOKUWEMO KATIKA NDEGE HIYO.
Waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak.
SHIRIKA la ndege la Malaysia limewaambia
jamaa na familia za abiria waliokuwa wanasafiri kwa ndege iliyotoweka
MH370 kwamba ndege hiyo imepotea na kwamba hakuna manusura. Tangazo hilo
limetolewa kwa familia hizo kwa njia ya ujumbe wa simu ya mkononi ,
ambao BBC iliweza kuuona.
Ndege ya Malaysia MH320 ilitoweka ikiwa
na abiria 239 baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur
tarehe 8 mwezi huu.
Aidha tangazo hilo limekuja huku juhudi za
kutafuta mabaki ya ndege hiyo Kusini mwa Bara Hindi zikimalizika kwa
siku ya tano bila mafaniko.
Waziri mkuu wa Malaysia amesema kuwa ndege hiyo ilianguka Kusini mwa Bahari Hindi, bila ya manusura wowote.
Aliambia
waandishi wa bahari kuwa udadisi uliofanyiwa data ya Satelite kutoka
Uingereza ndio umewathibitishia kwamba ndege hiyo ilimalizia safari yake
Magharibi mwa mji wa Perth mbali na eneo lolote la kutua.
Ameomba
vyombo vya habari kuheshimu familia za watu waliokuwa ndani ya ndenge
hiyo, akisema kuwa anasikitishwa sana kwani kipindi chote walichosubiri
taarifa njema , mwishowe imekuja kuwa taarifa mbaya hata zaidi.
Ndege
ya Malaysia MH-370, ilipoteza mawasiliano wiki mbili zilizopita. Ndege
na meli za nchi mbali mbali zimekuwa zikitafuta angalau mabaki ya ndege
hiyo bila ya kupata chochote.
BBC