Share this Post

dailyvideo

NEWS ALERT: Mkuu wa jeshi aponea kifo Somalia

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399


Jenerali Dahir anaendesha moja ya magari yenye uwezo mkubwa wa kudhibiti mashambulizi
Mkuu wa jeshi la Somalia ameponea chupuchupu kuuawa mjini Mogadishu.
Hili ndilo shambulio la punde zaidi katika msururu wa mashambulio dhidi ya viongozi wa serikali na rasilimali za serikali nchini humo.
Gari lake Jenerali Dahir Aden Elmim lilirushiwa bomu katika barabara kuu karibu na afisi za wizara ya ulinzi mjini Mogadishu.
Aliponea kwa sababu yeye huendesha mojawepo ya magari machache yaliyo na uwezo wa kudhibiti shambulio la risasi, ambayo yametengewa viongozi wakuu wa serikali hiyo.
Hakuna yeyote aliyedai kuhusika na shambulio hilo kufikia sasa japo inafahamika kuwa kundi la Al shabaab limekuwa likifanya mashambulio ya mara kwa mara mjini Mogadishu.
Mwishoni mwa juma, watu 15 waliuawa katika shambulio lililolenga jengo la bunge la Somalia. Wengine wengi walijeruhiwa wakiwemo wabunge 3.

BBC SWAHILI

Posted by Editor on 14:53. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for NEWS ALERT: Mkuu wa jeshi aponea kifo Somalia

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery