Share this Post

dailyvideo

Stars yatuma salamu Zimbabwe

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Na Sosthenes Nyoni,
Dar es Salaam. Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imetuma salamu Zimbabwe baada ya kuichapa Malawi kwa bao 1-0 jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kiungo wa Simba, Amri Kiemba aliifungia Stars bao pekee dakika 36 akimalizia kazi nzuri ya Shomari Kapombe, Kelvin Friday na Simon Msuva. Huo ni ushindi wa pili kwa kocha Mart Nooij tangu alipopewa jukumu la kuinoa Stars mwanzoni mwa mwezi huu.
Taifa Stars inajiandaa na mechi yake ya marudiano dhidi ya Zimbabwe itakayopigwa Juni Mosi jijiniHarare katika kutafuta kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika 2015.
stars pics
Kikosi cha stars
Taifa Stars iliuanza mchezo huo kwa kasi na dakika ya 16, Friday lililopaa juu kidogo ya lango la Malawi. Kiemba naye alikosa bao dakika ya 20, baada ya shuti lake kupaa juu kidogo ya lango la Malawi.
Kiemba alijirekebisha na dakika ya 36 aliifungia Stars bao la kuongoza kwa shuti baada ya pasi safi kati ya Shomari Kapombe, Friday na Msuva. Stars walikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao hilo moja, lakini pamoja na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga, washambuliaji wake walionekana kukosa umakini katika umaliziaji.
Kocha wa Stars, Nooij aliwapumzisha Msuva na Himid Mao na kuwaingiza Ramadhani Singano na Haruna Chanongo kipindi cha pili.
Malawi nusura wasawazishe bao dakika ya 60, wakati Chimango Kaira aliposhindwa kumalizia pasi nzuri ya Bashir Maunde.
Chanzo: Mwananchi

Posted by Editor on 15:27. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Stars yatuma salamu Zimbabwe

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery