Share this Post

dailyvideo

NGOMA ZA BAIKOKO, KANGAMOKO NA VIGODORO ZA PIGWA MARUFUKU DAR ES SALAAM.

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es salaam limepiga marufuku ngoma za kitamaduni ambazo zimekuwa zikifanyika  nyakati za usiku kwenye maeneo mbalimbali Dar es salaam ikiwa ni muendelezo wa kukabiliana makundi ya kihalifu ambayo yamekua tishio kwa usalama wa raia.
Kufuatia kuibuka kwa makundi ya kihalifu kama Panya road na Mbwa mwitu ambayo wengi wao wanahusishwa na ngoma hiyo kwenye uporaji na upigaji wa watu, Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Suleiman Kova anasema ‘ni marufuku kwa ngoma yeyote ya asili kuchezwa nyakati za usiku’

Kamanda Kova anasema kufuatia operesheni inayoendeshwa dhidi ya vikundi hivyo vya kihalifu, mpaka sasa tayari wanawashikilia wafuasi zaidi ya mia moja ambapo pia watu wengi wamekuwa wakilalamikia vitendo viovu vinavyofanyika nyakati za usiku wakati wa ngoma hizo maarufu kama ‘vigodoro’ pamoja ‘baikoko’ na sasa jeshi la polisi limetoa onyo kali kwa watakaoendeleza hizi ngoma kuanzia sasa.

Posted by Editor on 14:47. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for NGOMA ZA BAIKOKO, KANGAMOKO NA VIGODORO ZA PIGWA MARUFUKU DAR ES SALAAM.

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery