Sudan Kusini:Mazungumzo yatibuka Ethiopia
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Mazungumzo ya ana kwa ana kati ya wawili hao bila shaka yatakuwa hatua nzuri kwa mchakato huo wa amani.
Mkutano huo wenyewe utakuwa wa kwanza kwa viongozi hao kukutana tangu kutia saini makubaliano ya amani tarehe 9 mwezi Mei na wa pili tangu mwezi Januari.

Waziri wa mawasiliano Michael Makuei, alisema katika taarifa yake kuwa serikali ina matumaini kwamba awamu hii ya mazungumzo itafaulu na kwamba amani itapatikana.
Wakati huohuo, shirika la Amnesty International limewasihi wapatanishi kutoruhusu msamaha kwa washukiwa wa uhalifu kujumuishwa kwenye mkataba wa amani, na pia kuwaadhibu wale watakaopatikana na hatia ya kutenda uhalifu wa kivita.
Umoja wa Mataifa umetuhumu pande zote kwenye mzozo huo kwa kutenda uhalifu wa kivita na kutoa wito kwao kuheshimu mkataba wa amani.
Mashirika ya misaada pia yanaonya dhidi ya kuzorota kwa hali ya kibinadamu na tisho la ukame ikiwa vita vitaendelea.
