Share this Post

dailyvideo

Sudan Kusini:Mazungumzo yatibuka Ethiopia

Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Waasi nchini Sudan Kusini bado wanaendelea kupigana na majeshi ya serikali
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir pamoja na kiongozi wa waasi Riek Machar wanatarajiwa kukutana Jumanne katika juhudi za kumaliza mzozo wa kisiasa ambao umekumba nchi hiyo kwa miezi sita.
Mkutano wao uliotarajiwa kufanyika leo mjini Addis Ababa ulitibuka baada ya viongozi waliotarajiwa kwenye mazungumzo hayo kukosa kufika.
Duru zinaarifu kuwa mazungumzo hayo mjini Addis Ababa kati ya mahasimu hao yatafanyika Jumanne mchana kwa ushirikiano na viongozi wa kikanda kutoka shirika la IGAD.
Mazungumzo ya ana kwa ana kati ya wawili hao bila shaka yatakuwa hatua nzuri kwa mchakato huo wa amani.
Mkutano huo wenyewe utakuwa wa kwanza kwa viongozi hao kukutana tangu kutia saini makubaliano ya amani tarehe 9 mwezi Mei na wa pili tangu mwezi Januari.
Hali inayokumba wananchi wa Sudan Kusini
Lakini makubaliano ya kusitisha vita yamevunjika mara kwa mara huku mapigano yakiendelea katika nchi hiyo changa na kuzorotesha mgogoro huo ambao tayari umesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimisha wengine milioni moja nukta tatu kutoroka makwao.
Waziri wa mawasiliano Michael Makuei, alisema katika taarifa yake kuwa serikali ina matumaini kwamba awamu hii ya mazungumzo itafaulu na kwamba amani itapatikana.
Wakati huohuo, shirika la Amnesty International limewasihi wapatanishi kutoruhusu msamaha kwa washukiwa wa uhalifu kujumuishwa kwenye mkataba wa amani, na pia kuwaadhibu wale watakaopatikana na hatia ya kutenda uhalifu wa kivita.
Umoja wa Mataifa umetuhumu pande zote kwenye mzozo huo kwa kutenda uhalifu wa kivita na kutoa wito kwao kuheshimu mkataba wa amani.
Mashirika ya misaada pia yanaonya dhidi ya kuzorota kwa hali ya kibinadamu na tisho la ukame ikiwa vita vitaendelea.
 BBC

Posted by Editor on 19:50. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0

0 comments for Sudan Kusini:Mazungumzo yatibuka Ethiopia

Post a Comment

Recent Entries

Recent Comments

Photo Gallery