Watu saba wakamatwa kwa dhuluma za ngono Misri
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399

Wiki jana Misri ilifanya dhuluma za kingono kuwa uhalifu ambao adhabu yake ni miaka 5 jela
Wanaume saba wamekamatwa nchini
Misri, baada ya kushukiwa kuwadhulumu kiongono wanawake katika sherehe
za Jumamosi za kumkabidhi rasmi mamlaka Rais Abdul Fattah al Sisi.
Hatua ya kuwakamata wanaume hao, inakuja baada
ya kanda ya video kusambazwa kwenye internet ikionyesha mwanamke
akivuliwa nguo na kuvamiwa na genge la wanaume
Haijulikani ikiwa kanda hiyo ilinaswa, lakini
walioshuhudia kitendo hicho waliambia BBC kwambwa unyama huo ulitokea
Jumapili usiku.
Wiki jana maafisa wa utawala nchini Misri,
waliharamisha dhuluma za kingono na kuufanya uhalifu kwa mara ya kwanza
adhabu yake ikiwa miaka mitano jela kwa watakaopatikana na hatia.
BBC

Posted by Editor
on 19:55.
Filed under
worldnews
.
You can follow any responses to this entry through the
RSS 2.0