RAIS UHURU KENYATA WA KENYA AWA RAISI WA KWANZA KUPANDA DALADALA KUTOKA OFISINI KWENDA MJINI
Ikiwa unatukio Lolote au Habari yoyote usisite kututumia kupitia Barua Pepe blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba yetu +255765056399
Rais uhuru Kenyata ameendelea kujizolea umaarufu mkubwa nchini Kenya kutokana na matukio mengi anayoyafanya, mengi yakiwa yale ambay ni mara chache sana kumuona rais akifanya. Mfano ni kama lile tukio la kutoka ikulu akiwa hana bila ya walinzi, kucheza mziki katika matamasha mbalimbali na lile la kusimamisha msafara wake kisa tu anunue karanga.
Jipya alilolifanya siku ya jana ni pale alipoamua kutumia usafiri wa Matatu au kwetu tunaita Daladala kwenda mjini. Inasemekana Rais Kenyata ndio rais wa kwanza ktumia usafiri huo akiwa madarakani, marais wote waliopita hawajawahi kuutumia wakiwa madarakani. Kikubwa kingine alichosema na kimeungwa mkono na vijana wengi ni kuruhusu Daladala kuchorwa Graffit jambo ambalo limekua likizuiliwa na uongozi nchini humo kwa mda sasa. Rais Kenyata alisema ” To be frank why are we interfering with graffiti on Matatu? Let us promote our young people – Uhuru Kenyatta ”
You might also like:
Posted by Editor
on 20:47.
Filed under
eastafricannews
.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
Nimempenda bure! Safi Sana wengine wanatakiwa kuiga mfano. Binafsi nilifarijika zaidi alipotoa msaada kwa raia wake alipomtumia text message bila kusita akampigia simu haraka Na kumsaidia. Yan viongozi wote wangekua hivi daaaa! Tungepata raha Sana.